Tunaweza kujitosheleza kwa Sukari
Tunaweza kujitosheleza kwa Sukari
Leo siku nzima kamati ya PAC ilikuwa inazungumza na Bodi ya Sukari, Wizara ya Kilimo na Wakulima wa Miwa Wilayani Kilombero. Tanzania huzalisha wastani wa tani 300,000 za Sukari kwa mwaka ilhali mahitaji ni tani 420,000 kwa mwaka. Hii hupelekea uagizaji wa Sukari kutoka nje ambao umekumbwa na malalamiko makubwa sana kutoka kwa wadau mbalimbali.
Masuala kadhaa yameibuliwa katika kikao cha leo
- Wakulima wamelalamikia sana uingizaji holela wa Sukari nchini. Bei ya Miwa imeshuka kutoka tshs 69,000 kwa tani mpaka tshs 55,000 sababu ya Sukari ya ndani kukosa soko.
- Wakulima wamelalamikia viwanda kwa kujipangia bei bila kuwashirikisha wao na pia viwanda ndio vinapima Miwa na ubora wa mua wa mkulima hivyo kuleta mgongano mkubwa wa MASLAHI kwa mwekezaji
- Wakulima wametaka hisa 25% za Serikali katika viwanda vya Sukari wapewe wao ili waweze kushiriki katika Uchumi wa nchi
- Bodi ya Sukari imeshindwa kuendeleza mradi wa RUIPA kwa sababu ya kutokuwa na Fedha tshs 11 bilioni za kulipa fidia ya Wananchi katika eneo la mradi. Mradi huu ungeweza kuzalisha tani 244,000 za Sukari kwa mwaka
- Wakulima wamelalamikia sana tabia ya viwanda kushindwa kununua Miwa yote ya Wakulima na hivyo kupelekea takribani nusu tu ya Miwa kutumika na nusu nyingine kubaki mashambani na kuharibika. Wastani wa tani 400,000 za Miwa huharibika Wilayani Kilombero peke yake. Hii ni sawa na tani 50,000 za Sukari
PAC imetoa ufafanuzi wa masuala yafuatayo
- Kamati ilikwishaiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania kufanya uchunguzi wa kikodi katika Sekta nzima ya Sukari nchini. TRA wameijulisha kamati kwamba wanafanyia kazi suala hilo na wameomba muda zaidi ili kukamilisha kazi hiyo. PAC imekubaliana na ombi hilo na pia kwamba inasubiri Taarifa ya kikosi kazi kilichoundwa na Katibu Mkuu Kiongozi ili kupata suluhisho la kudumu la Changamoto zinazokabili Sekta ya Sukari. Kamati ikishapata taarifa zote hizo itazifanyia kazi na kuziwasilisha Bungeni.
- Kamati imeielekeza Bodi ya Sukari kuhakikisha inaendeleza mradi wa RUIPA kwa kutangaza zabuni ya kumpata mwekezaji ambaye atalima sehemu ya shamba na kumilikisha kwa hati Wakulima ( outgrowers) sehemu nyingine ya shamba. Mradi wa RUIPA uwe mfano wa ushiriki wa wananchi katika Kilimo cha kisasa. Wakulima wamilikishwe Ardhi ya kulima Miwa na kuuza kwenye kiwanda, wasikodishiwe Ardhi hiyo. Bodi ya Sukari ipate FEDHA tshs 11 bilioni za fidia ya wananchi kutokana na zabuni ya kupata mwekezaji na malipo tangulizi ya mwekezaji.
- Modeli ya Malaysia yaweza kutumika katika mradi wa RUIPA, kwa kuwagawia wananchi ( households ) 1500 wanaoathiriwa na mradi kila mmoja hekta 5 ( 4 za kulima Miwa na 1 ya makazi yake ) na hekta zinazobakia katika jumla ya hekta 14700 ziwe nucleus. Ushiriki wa wananchi katika uzalishaji wa Ndio njia endelevu ya kutokomeza umasikini nchini.
- Kamati imeelekeza kuwa Bodi ya Sukari iwe na mamlaka ya kuwa mdhibiti ( regulator ) kwa kutoa bei elekezi za mauzo ya Miwa na Sukari nchini ili kulinda Wakulima dhidi ya unyonyaji wa wawekezaji. Bodi pia ihusike na udhibiti katika upimaji wa Miwa na kiwango cha Sukari katika Miwa ( sucrose ) ili kujibu Changamoto ya Wakulima kupunjwa.
- Kamati imeelekeza kuwa vianzishwe viwanda vya ngazi ya kati vya Sukari ili kutumia Miwa ya ziada na kuzalisha Sukari na hivyo kuongeza uzalishaji. Vyama vya Wakulima wa Sukari vimehamasishwa kuanzisha viwanda vidogo hivyo na Bodi ya Sukari imeelekezwa kulegeza masharti ya uanzishaji wa viwanda vya ngazi ya kati.
- PAC imepingana na Wakulima kwamba hisa za Kampuni 25% wapewe wao na badala yake PAC imeelekeza Msajili wa Hazina aangalie uwezekano wa kuorodhesha hisa za Serikali katika soko la hisa la Dar Es Salaam na vyama vya Wakulima vipewe fursa kununua sehemu ya hisa hizo ( angalau 5%).
- Wakulima wa Miwa wamehamasishwa kujiunga na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ili wafaidike na mafao ya muda mrefu na muda mfupi ikiwemo Bima ya Afya, mikopo katika SACCOS zao na pensheni uzeeni. Tanzania ina jumla ya Wakulima wa Miwa ( out-growers ) 19,000 wenye kuzalisha nusu ya Sukari inayozalishwa nchini.
Tukipunguza upotevu wa Miwa ya Sukari ( wastage ) nchi nzima kwa kuanzisha viwanda vya Kati vya kusindika Miwa, tunaweza kuongeza uzalishaji kwa zaidi ya tani 80,000 za Sukari na kupunguza Sukari inayoagizwa kutoka nje. Tukitekeleza mradi wa RUIPA, tutakuwa na Sukari ya ziada tani 200,000 ambazo tunaweza kuuza nje na kupata fedha za kigeni.
Hii iwe mikakati ya muda mfupi. Tunaweza tukiamua na kashfa za Sukari zitakuwa Historia. Tufanye sasa
Azimio la Mtwara -Uwajibikaji katika Uvunaji wa Maliasili ya Nchi yetu
Azimio la Mtwara
Uwajibikaji katika Uvunaji wa Maliasili ya Nchi yetu.
Tanzania kama zilivyo nchi nyingi za bara la Afrika imejaaliwa kuwa na Rasilimali mbali mbali za asili. Miongoni mwa rasilimali hizo ni pamoja na Madini na Gesi Asilia. Usimamizi wa uvunaji wa rasilimali hizi umegubikwa na manung’uniko makubwa ya wananchi hususan kutokana na usiri mkubwa uliopo kwenye mikataba ya uvunaji wa Maliasili hizi za Taifa. Mikataba yote 6 ya uvunaji wa Dhahabu bado ni Siri kubwa na vile vile mikataba yote 26 ya utafutaji na uvunaji wa Gesi Asilia na Mafuta. Mikataba miwili imevuja mpaka sasa na yote imeonyesha tofauti kubwa sana na mikataba ya mfano ambayo Serikali imeweka wazi. Mikataba ya mfano hutumika kujadiliana na makampuni ya uwekezaji katika utafutaji na uchimbaji wa Gesi na Mafuta hapa nchini. Mageuzi katika sekta ndogo ya gesi na mafuta yamekuwa hayashirikishi wananchi na hufanywa kwa usiri mkubwa na hivyo kusababisha wananchi kutokuwa na taarifa kabisa na kinachoendelea katika utajiri wao wa asili.
Mwaka 2007 nilitangaza Azimio la Songea lililokuwa na malengo makuu manne
1) kutokuwa na mikataba mipya ya madini mpaka mikataba iliyokuwepo ipitiwe. Mikataba yote ya madini ilipitiwa na Kamati ya Bomani na tangu mwaka 2007 hapajawa na mkataba Mpya wa madini ulioingiwa na Serikali.
2) kufanya mabadiliko ya sheria zote za kodi ambazo ni kikwazo katika kukusanya kodi katika sekta ya madini. Sheria husika zimefanyiwa marekebisho ikiwemo kupandisha mrahaba, kufuta nafuu ya kodi ya ongezeko la thamani kwa kampuni za madini na kuirejesha kodi ya ongezeko la mtaji.
3) Serikali kumiliki sehemu ya hisa katika migodi ya madini. Kwa mujibu wa sera Mpya ya madini ya mwaka 2009 na sheria Mpya ya madini ya mwaka 2010 Serikali itakuwa na hisa katika kila mgodi Mpya unaoanza nchini.
4) Halmashauri za Wilaya zenye migodi kupata mgawo wa theluthi ya mrahaba unaokusanywa katika madini yanayovunwa nchini. Pamoja na kwamba hivi sasa Halmashauri zinakusanya kodi ya ‘ cess’ lakini bado Serikali Kuu inabeba fedha yote ya mrahaba.
Malengo haya yaliongoza mjadala wa masuala ya madini mwaka 2007 mpaka 2010 sheria Mpya ya madini ilipotungwa. Utekelezaji wa Azimio la Songea ni wa zaidi ya 75% lakini bado kilio cha wananchi kipo pale pale. Hii inatokana na usiri mkubwa wa mikataba na hususan mikataba ya gesi na miundombinu yake. Usiri huu unasababisha ukosefu mkubwa wa uwajibikaji kwa upande wa watendaji wa Serikali. Usiri hupelekea rushwa na ufisadi. Moja ya sababu kubwa zinazotolewa na watetezi wa usiri wa mikataba ni kwamba mikataba ile ina Siri za kibiashara na hivyo washindani wa kibiashara wataiba Siri za wenzao. Hoja hii ni nyepesi sana kwani makampuni yote makubwa yanayowekeza nchini yamesajiliwa katika masoko ya hisa kwenye nchi za magharibi na katika masoko hayo mikataba yao hulazimika kuwekwa wazi. Hivyo usiri huo ni kwa wananchi tu na sio kwa hao washindani. Makampuni mengi yaliyopo nchini yanamilikiwa na watu wale wale kupitia masoko ya hisa. Vile vile majirani zetu kama Msumbiji wameweka mikataba yao yote wazi.
Ni dhahiri kwamba moja ya sababu kubwa ya kushamiri kwa rushwa nchini kwetu ni ukosefu wa mfumo thabiti wa uwajibikaji. Ndio maana katika mkutano wa kufunga mwaka 2014 na kuukaribisha mwaka 2015 uliofanyika mjini Mtwara tarehe 31 Desemba 2014, niliwaomba wananchi wa Mtwara kuufanya mwaka 2015 kuwa ni mwaka wa kuwajibishana. Hivyo Azimio la Mtwara ni wito wa kutaka Uwazi na Uwajibikaji katika utafutaji na uvunaji wa mali asili za nchi yetu. Azimio la Mtwara lina malengo yafuatayo
1 kutaka mikataba yote inayohusu uvunaji wa rasilimali za nchi iwekwe wazi kwa wananchi na Bunge liipitie kuidhia kabla ya kuingiwa kwa mikataba hiyo
2 kutaka haki ya wananchi kuruhusu utafutaji wa madini au gesi na mafuta katika maeneo yao ( right of free prior informed consent )
3 kutaka sehemu ya mrahaba unaotokana na uvunaji wa Maliasili ya nchi kugawanywa kwa maeneo yanayovunwa rasimali hizo
4 kutaka mfumo wa mapato na matumizi ya mapato yasiyo ya kikodi ( rents ) yanayotokana na uvunaji wa Maliasili za nchi kuwa wazi kwa wananchi na kushirikisha wananchi katika kupanga matumizi husika kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo
Azimio hili ni wito tu utakaotusaidia kuiwajibisha Serikali katika masuala ya utajiri wa Taifa.
Zitto Kabwe, Mb
Mtwara 31-12-2014
Kwanini Bei ya mafuta kwa walaji haishuki kwa kasi?
Kwanini Bei ya mafuta kwa walaji haishuki kwa kasi?
Kuanzia Mwezi Julai mwaka 2014 mpaka Desemba, bei ya mafuta ghafi imekuwa ikishuka kutoka $110 kwa pipa mpaka $56 kwa pipa. Mporomoko huu wa bei wa zaidi ya 40% haujaleta unafuu kwa mtumiaji wa kawaida wa mafuta ikiwemo wenye daladala na kupelekea nauli za usafiri wa umma kupungua. Leo bado bei ya mafuta kwenye vituo vya mafuta ni tshs 2029 kwa Petroli na 1909 kwa dizeli, bei ambayo ni karibia ile ile kwa miezi michache iliyopita.
EWURA,inasemekana, wamesema kuwa bei za hapa nchini hushuka baada ya miezi 2 kwa sababu waagizaji huagiza kwa ujumla mafuta mengi zaidi na hivyo kutofaidika na punguzo la bei. Hata hivyo bei zimeanza kushuka toka mwezi Julai na hatujashuhudia unafuu wowote kwa wananchi. Ingekuwa bei ya mafuta imepanda tungeona bei zimepanda mara moja na sababu za kununua ‘ bulky’ huwa hazitolewi.
Ni kweli kwamba Tanzania hununua mafuta yaliyosafishwa na hivyo bei inayoshuka sio hiyo. Lakini hao wasafishaji hununua mafuta ghafi yenye bei ndogo hivi sasa kwa hiyo ni dhahiri lazima bei za pampu zipungue. Vile vile ni kweli kwamba thamani ya shilingi ya Tanzania imeporomoka hivyo wananchi hawawezi kuona unafuu wa bei ya mafuta kwa sababu hununuliwa kwa fedha za kigeni na kuuzwa kwa Sarafu yetu. Hata hivyo kasi ya kushuka kwa bei ya mafuta ni 40% wakati shilingi imeshuka kwa chini ya 10%. Katika hali ya kawaida na kwa kutumia mfumo wa kukokotoa bei wa EWURA, angalau bei ya mafuta ingeshuka kwa kati ya 15% and 25%.
Ni dhahiri mamlaka za nchi na hasa EWURA wanapaswa kueleza kwa umma ni Kwanini bei za mafuta hazishuki kulingana na bei ya bidhaa hiyo katika soko la Dunia. Wananchi wana haki ya kujua na kama hakuna Maelezo basi bei hizo zishuke na wananchi wafaidike na punguzo hilo.
Zitto Kabwe, Mb
RATIBA -KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC) JANUARI 2015
KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC)
RASIMU YA RATIBA YA UKAGUZI WA MIRADI NA KUJADILI HESABU ZILIZOKAGULIWA ZA SERIKALI KUU NA MASHIRIKA YA UMMA KUANZIA TAREHE 05 HADI 24 JANUARI 2015,
MKOA WA MOROGORO NA OFISI NDOGO YA BUNGE, DAR ES SALAAM
Vitabu Nilivyosoma 2014 – Books I have read in 2014 #BooksRead2014 #letsread
Mwaka 2014 nimesoma vitabu 53 na nimefanya uchambuzi wa vitabu 21 kupitia safu ya Kitabu na Kalamu ya gazeti la Raia Tanzania kila Jumatatu.
Tangu nimeanza utaratibu kuchapisha idadi ya vitabu nilivyosoma huu ni mwaka wa tatu sasa. Mwaka 2012 nilisoma vitabu 31, mwaka 2013 vitabu 13 na 2014 vitabu 53.
Mwaka 2014 niliuanza kwa changamoto nyingi sana katika maisha yangu ya kisiasa; kuvuliwa nyadhifa katika chama na kuwa hatarini kuvuliwa uanachama kilichopelekea kwenda mahakamani kutetea uanachama wangu. Vile vile kuanzia mwezi Machi nilianza kumwuguza mama yangu mzazi mpaka mungu alipomchukua hapo mwezi Juni. Muda mwingi niliutumia kusoma vitabu kama matibabu ya msongo ( therapy ). Mchakato wa Katiba ( ambao sikushiriki kwa sababu ya kuona dhahiri hautaleta katiba bora ) pia ulinipa muda mzuri wa kufanya jambo ninalolipenda kuliko yote – Kusoma.
Kitabu kimoja (ADAPT) kimenifanya kubadili kabisa mtazamo wangu wa maisha.
Vitabu 2 ( Exposure na Munyakei story ) vilinitia faraja kubwa katika kazi niliyokuwa nafanya tangu mwezi Machi ( uchunguzi wa akaunti ya #TegetaEscrow ).
Kitabu kimoja ( The myth of the strong leader ) kimepanua sana uwezo wangu katika kuchambua viongozi na mafanikio yao. Vyote nilifanikiwa kuvifanyia uchambuzi katika RaiaTanzania.
Bado India imechomoza sana katika orodha yangu. Miezi 2 niliyokaa Madras kumtibu mama imechangia sana kuongeza vitabu kutoka waandishi wa India. Vingi ni fiction. India Calling kilinivutia zaidi kuliko vyote. Mwaka 2014 nimeanza kusoma kazi za ushairi za zamani (Classics) ili kupata maarifa mengi yaliyojaa kwenye ushairi na kuendeleza ujuzi wa kuandika mashairi.
Kitabu kimoja nilikianza nikashindwa kukimaliza, The Capital. Mungu akipenda nitakimaliza mwaka 2015. Karibu katika orodha yangu ya vitabu mwaka 2014.
Zitto Kabwe, MB
BOOKS THAT I HAVE READ IN 2014
TAARIFA YA KAMATI KUFUATIA MATOKEO YA UKAGUZI MAALUM WA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KATIKA AKAUNTI YA TEGETA ESCROW ILIYOKUWA KATIKA BENKI KUU YA TANZANIA
TAARIFA YA KAMATI KUFUATIA MATOKEO YA UKAGUZI MAALUM WA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KATIKA AKAUNTI YA TEGETA ESCROW ILIYOKUWA KATIKA BENKI KUU YA TANZANIA
Nashambuliwa, tunashambuliwa! PAC tunasema “Hatutetereki”
Nashambuliwa, tunashambuliwa! PAC tunasema “Hatutetereki”
Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya Kamati ninayoongoza ya PAC kuwasilisha Bungeni Taarifa Maalumu kuhusu ukaguzi maalumu wa akaunti ya Tegeta Escrow, kumekuwa na kampeni za chini chini zinazoendeshwa kwenye korido za Bunge na kwenye mitandao dhidi yangu binafsi na baadhi ya wabunge waliosimama kidete dhidi ya wizi wa fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania akaunti ya Escrow.
Baadhi ya tuhuma nimezipeleka kwenye vyombo vya dola ili zichunguzwe kwani zina vielelezo vya mahala pa kuanzia (kama leseni ya udereva ya mwanamke anajulikana kama Vivian Emmanuel Sirikwa na muhuri wa kampuni ya uwakili inayomilikiwa na Bwana Joseph Mkandege).
Baadhi ya tuhuma nitazijibu moja baada ya moja.
Waziri mmoja ambaye ni mtuhumiwa wa wizi wa fedha za Tegeta Escrow anazunguka kwa wabunge akisema tuhuma hizi kupikwa kama njia yake ya kuhamisha mjadala kutoka uporaji wa Tshs 200 bilioni kwenda kwenye masuala binafsi.
Tuhuma hizi zenye kichwa cha habari “Zitto na Filikunjombe wanatumiwa na Kenya na Uingereza kuvuruga na kudhoofisha Uwekezaji nchini mwetu” zinajibiwa hapa chini. Utaona ndugu Filikunjombe ametajwa kwa kichwa cha habari ili kumtaja tu bila sababu yeyote ile.
Tuhuma #1:
Zitto anaye rafiki yake Mkenya aitwae Rapahel Ongangi ambao kwa pamoja wameanzisha Gombe Advisors Co. Ltd (registered on 24 November 2011, Certificate No 87387) kwa ajili ya kufanya biashara na Makampuni ya Gesi na Mafuta yanayofanya kazi nchini hapa.
Majibu:
Gombe Advisors ni kampuni binafsi isiyofanya faida yaani ‘Company Limited by Guarantee’. Haina kazi na kampuni yoyote ya Gesi na Mafuta na wala yenyewe haijuhusishi na biashara hiyo. Gombe advisors haijafanya kazi yoyote ile na kampuni nyingine zaidi ya kusaidia wasanii wa kundi la Kigoma All stars. Upotoshaji hapa unalenga kupindisha mjadala.
Tuhuma #2:
Zitto amemsaidia Ongangi kupata uraia wa Tanzania na kwa sasa ni raia wa pasipoti. Zitto na Ongangi walimtafutia CEO wa Shell aitwae Axel Knospe nyumba na gari ya kukodi.
Majibu:
Raphael ni mtu binafsi ambaye anafanya shughuli zake hapa nchini, amesoma hapa nchini na ameoa na ana mtoto. Tuhuma hizi hazina msingi wowote ule maana ni uwongo. Wanaotoa tuhuma hizi waonyeshe hiyo pasipoti ya Bwana Ongangi kuthibitisha madai yao.
Tuhuma #3:
Mikataba ya STATOIL iliyokuwa inarushwa kwenye mitandao ya jamii na kuchapishwa kwenye magazeti ya Kenya ya hapa nchini (The Citizen na Mwananchi) mwandishi mkuu alikuwa huyo CEO wa Shell.
Majibu:
Mkataba uliovujishwa wa StatOil ulivujishwa na waandishi wa habari wa Norway. Uchambuzi wa mkataba huo nimeufanya mwenyewe kwa kutumia utaalamu wangu niliosomea wa kuchambua mifumo ya kodi kwenye sekta ya mafuta na gesi. Kwa namna yoyote ile, huyo anayetajwa kuwa CEO wa kampuni ya Shell hahusiki. Tuhuma hii wanaoitoa watoe ushahidi usio na chembe ya mashaka.
Ikumbukwe kuwa mkataba wa StatOil utaipotezea Tanzania mapato ya dola za Marekani bilioni 12 (takribani Tshs 20,400,000,000,000/=) katika kipindi cha miaka 15 baada ya gesi kuanza kuchimbwa.
Uamuzi wa Kamati ya PAC kutaka mikataba yote ya Gesi kuwa wazi una lengo la kuchambua kuona kama mikataba yote nchini haipotezi mapato kwa nchi. Uamuzi huo umewakasirisha sana baadhi ya waliohusika kuingia mikataba Serikalini maana wanajua kuna madudu kwenye mikataba na wanataka umma wa watanzania usijue!
Tuhuma #4:
Kampuni ya SHELL imechukizwa sana kucheleweshwa kwa kupata kibali cha kutafuta gesi na mafuta kule Pemba. Vilevile SHELL haina uwekezaji mkubwa Tanzania Bara kwani ilishindwa kwenye tenda zenye vitalu vyenye gesi nyingi upande wa Bara.
Majibu:
Ukweli ni kuwa Kampuni ya Shell ina vitalu 4 huko Zanzibar na tayari ina makubaliano na Serikali ya Zanzibar kuhusu utafutaji mafuta huko katika vitalu namba 9,10,11 na 12. Shell inafanya kazi na kampuni ya Petrobras ya Brazil kwenye kitalu namba 6 na namba 8. Taarifa hizi zipo wazi kwenye tovuti ya TPDC. Tuhuma nyepesi namna hii dhidi ya kampuni kubwa kama Shell zinaonyesha dharau na kiburi kinachotokana na uelewa mdogo wa mambo wa watu wanaotuhumu.
Tuhuma 5:
Ongangi anapokea maelekezo kutoka Serikali ya Kenya kuhujumu uwekezaji nchini mwetu.
Majibu:
Nazifahamu mbinu nyingi zinazotumika kufanya propaganda, lakini mbinu hii imeshindwa ikiwa mapema sana. Ni vema wanaotoa tuhuma hizi wazithibitishe vinginevyo ni mwendelezo wa propaganda zisozingatia diplomasia ndani yake dhidi ya jirani zetu wa Kenya. Hizi ni propaganda hatari ambazo hata hao wanaotuhumiwa wakisikia watatudharau sana.
Tuhuma #6 (juu ya Uingereza):
Uingereza imekuwa inamfadhili Zitto kwa miaka mingi kwa mambo yake ya kisiasa kwa hiyo sasa hivi Ubalozi wa Uingereza unamlipa Zitto na Kafulila kuhakikisha kwamba Standard Chartered ya Uingereza inalipwa deni lake lisilotambulika kisheria nchini mwetu.
Majibu:
Nimetangulia kusema hapo awali kuwa kuna propaganda ambazo haziangalii hata diplomasia; nyingine ni hii. Pamoja na kukanusha uzushi huu, ni vizuri wanaotoa tuhuma za namna hii kuthibitisha. Mimi binafsi sijawahi kufadhiliwa kisiasa na Taifa lolote lile. Inaelekea kuna wanasiasa wanaofadhiliwa na mataifa mengine ambao kwakuwa kwao ndiyo maisha wanaamini na wengine tupo kama walivyo.
Kwangu itikadi yangu ni ‘Uzalendo kwa nchi yangu’, ni jambo ambalo halina mbadala wake. Siku zote nasema “Right or wrong, my country first”.
Kurudia kurusha tuhuma kwa Ubalozi wa Uingereza nchini ni kudhihirisha kwa mara nyingine kiburi cha kuwa na mamlaka (arrogance of power) walicho nacho wanaotuma tuhuma hizi.
Aidha, wanatuhumu kuwa “Kafulila na Zitto wamehaidiwa 15% ya USD 150 million kama deni likilipwa”
Mtanzania anayeweza propaganda dhaifu kama hizi basi anatakiwa ajitafakari. Hata hivyo ni vema wanaotoa tuhuma hizi wathibitishe bila chembe ya mashaka.
Tuhuma #7:
Mbunge Mkono nae ameshikwa hasira kupoteza kazi ya uwakili pale TANESCO. Kafulila na Zitto wanalipwa na Mkono kuvuruga Serikali kwa hasira za kukosa fedha za kitapeli za TANESCO.
Majibu:
Hizi ni tuhuma ambazo sasa tumezizoea kutolewa. Mambo mepesi hayawezi kujibu mambo ya msingi kama tuhuma za wizi wa fedha zaidi ya Tshs bilioni 200 kutoka Benki kuu ya Tanzania. Kukusanya kila propaganda ili kuuhamisha umma ni kupungukiwa hekima na busara.
Aidha, wanaotuhumu wanadokeza kuwa “Naomba tuwe macho na Wabunge wetu achananeni na madai ya Zitto ya wizi. Huyu mtu anafanya biashara na Kampuni ya SHELL na inasemekana analipwa na Ubalozi wa Uingereza. Serikali ya Kenya na tapeli mkubwa Mbunge Mkono nae anawalipa Zitto na Kafulila”.
Watanzania, haya ni maneno ya hasira ya watu wanaokaribia kukamatwa kwa kushiriki wizi wa fedha katika Benki kuu ya Tanzania. Kamwe tuhuma kama hizi haziwezi kutukatisha tamaa katika kupambana ili ukweli ujulikane. Sisi tutapigana kwa ajili ya Taifa, kwa ajili ya mtanzania na tunachotaka ni umma uujue ukweli wa mambo.
Hasira hizi zinatokana na mambo mawili:
Moja ni uamuzi wa kamati ya PAC kuwasweka ndani baadhi ya watendaji wa TPDC kwa kushindwa kutekeleza maamuzi ya Kamati yanayohusu uwazi wa mikataba ya Gesi na Mafuta.
Pili, ni uamuzi wa PAC kuagiza ukaguzi maalumu wa mchakato mzima wa kuanzishwa na kufungwa kwa akaunti ya Tegeta Escrow ambapo zaidi ya shilingi bilioni 200 ziliporwa na zaidi ya shilingi bilioni 12 zinalipwa na TANESCO kila mwezi kwenda kampuni ya PAP inayomilikiwa na Harbinder Singh Seth (50%) na watu wasiojulikana kupitia kampuni ya Simba Trust iliyosajiliwa na kufichwa nchini Australia (50%).
Ieleweke kuwa PAP inalipwa shilingi milioni 400 kila siku kutoka TANESCO izalishe au isizalishe Umeme! Watanzania, PAP itaendelea kulipwa namna hiyo kwa miaka 20 ijayo. Kwa namna ambayo Seth analindwa na baadhi ya watendaji Serikalini na hasa ndani ya Wizara ya Nishati na Madini. Aidha, kuna fununu kuwa kuna maofisa serikalini wanaomiliki hizo 50% za kampuni ya PAP. Seth pia anamiliki kitalu cha gesi Mnazi bay Kaskazini kupitia kampuni ya HydroTanz.
Hasira hizi walizo nazo wanaonituhumu na Kamati yangu zimewapelekea kugushi nyaraka mbalimbali zinazonituhumu mimi na wenzangu ili kutuogopesha na kutukatisha tamaa katika kutafuta ukweli juu ya suala la uporaji wa fedha kutoka Benki kuu. Lengo lao ni kututoa kwenye mstari. Mimi na wenzangu hatutatoka kwenye mstari, tutashirikiana na wabunge wenzetu kuhakikisha ukweli unajulikana na wezi kuchukuliwa hatua kali.
Harbinder Singh Seth aliiangusha Serikali ya KANU nchini Kenya, sasa anachotaka kukifanya kinaweza kuiangusha Serikali ya CCM wakiendelea kumkumbatia.
Watanzania sio mabwege!
Zitto Kabwe
Mwenyekiti PAC
Dodoma, 9 Novemba 2014
Azama M Bwinza: The Audacity to Rescue 7 people from being drowned in Lake Tanganyika
Azama M Bwinza: The Audacity to Rescue 7 people from being drowned in Lake Tanganyika.
Saturday 11th October 2014 will remain a dark day for the people of Kigoma in general and Kigoma North constituency in particular, especially the villages of Mtanga, Kigalye and Kalalangabo Kagongo ward. Ten people drowned in Lake Tanganyika following the capsizing of twin canoes (mtumbwi wa kipe) with more than 50 people in it.
It was a celebratory day at the offset. There was a wedding ceremony in Mwandiga village and the bride and groom with relatives and friends were travelling to their new home in Kigalye village, which entailed travelling first by cars and ‘bodaboda’ and then crossing the lake in a twin canoe. The people in this area cannot afford hiring a boat so for many years, in community solidarity, fishermen offer their ‘mitumbwi’ to be used as transport for social events. Worse, villages along Lake Tanganyika North have only one means of transport which is waterways as no road has been built so far.
At around 1 pm that Saturday almost 50 people including the bride and groom got into the mitumbwi from Kalalangabo ferry and started to sail northward to Kigalye. 1pm after they set sail the mitumbwi turned upside down and what followed is now history.
Amongst the passengers was a 24 year old lady, Azama Mahmoud Bwinza. She is a widow with one child. She was the first to jump into the waters of this second deepest lake in the world and swam to shore. According to her story, she stood on the rocks at the shore to catch her breath and saw others trying to rescue themselves. She heard her younger sister calling out for help. Courage sank in and she dived back into the water. Knowing that Kalalangabo area is one of the deepest parts of the lake, she set off on her rescue mission.
‘I was holding people by their back and pulling them to the shore. I made seven trips and as a result I rescued 7 people including a pregnant woman and 3 children,’ Azama narrated. The last person she tried to rescue died. She was holding on to Azama so firmly that Azama couldn’t swim and both were at the brink of drowning. ‘I had to bite her to leave me or relax and I was exhausted. I went swam back to shore. The woman died.’ Azama explains while crying as the dead was her sister-in-law.
In whatever measure, Azama is the heroine of 2014 so far. The leadership she has shown is rare and her selfishlessness is worth emulating. If only our world had more Azamas.