Posts Tagged ‘Ziara Kanda ya Magharibi’
VIDEOS- Ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi #ChademaTV
Zitto: Mfumo wa Mikopo ya Elimu ya Juu inamnyima haki ya Elimu mtoto wa Mkulima
Zitto: Kwa hali niliyoiona Vijijini inabidi nitafakari upya kustaafu Ubunge
Zitto sijawa Kimya ni Propaganda tu
Siku ya Nne ya ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi -Wilaya ya Sikonge Mkoa wa Tabora
Siku ya Nne ya ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi imetupeleka Wilaya ya Sikonge Mkoa wa Tabora.
Nikiwa na Wenyeviti wa chama wa mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora pia Mwenyekiti wa Kanda ya Magharibi Ndg. Mambo tumefanya mikutano 4.
MAJI
Kata ya Kitunda nilivunjika moyo sana baada ya kushuhudia wananchi wakichota maji ya Kunywa kwenye dimbwi ambamo Ng’ombe anakunywa maji. Maji yana rangi kama chai ya maziwa. Nimevunjika moyo sana sababu kwa umri huu wa Taifa letu Maji safi na salama haipaswi kuwa ni jambo la kukampenia tena au kufanyia siasa. Kina mama wanatembea kilometa nyingi kwenda kuchimba maji kwenye madimbwi. Watanzania hawastahili kabisa maisha ya namna hii. Nimepata uchungu sana sababu hizi ndio kazi wanasiasa tunapasa kufanya kusaidia wananchi na kwa kweli kukutana na hali kama hii kunavunja moyo sana.
Baadhi ya Wabunge tulisimama kidete kuhakikisha bajeti ya Wizara ya Maji inaongezwa na ikaongezwa TZS185 bilioni kwa ajili ya Maji vijijini. Ni wajibu wetu wabunge kuhakikisha fedha hii inafika kwa wananchi ili kuwaondolea madhila haya wasiostahili. Changamoto kama hizi za wananchi masikini wa vijijini zinanifanya nifikirie sana nafasi yangu binafsi katika siasa za nchi yetu, siasa za masuala na majawabu.
Kero ya Wakulima wa Tumbaku
Kero ya wakulima wa Tumbaku bado ni kubwa sana na tumekuwa tunaelezwa kila tunapokwenda. Hapa Sikonge mwaka 2012/13 Chama Kikuu cha Ushirika kimewakata wananchi fedha za mbolea ambayo wananchi hawakupata. Wananchi wanakaa msimu mpaka msimu kupata fedha za mauzo ya Tumbaku. Makato ni mengi na kufanya mkulima ashindwe kuvunja mzunguko wa umasikini.
Nimetoa mawazo ya kisera kwamba imefikia wakati wakulima kupitia vyama vya msingi wajiunge na mifuko ya hifadhi ya jamii ili kuweza kwanza kuweka akiba, pili kupata mikopo nafuu kupitia vyama vyao vya kuweka na kukopa na hivyo kuweza kuwalipa wakulima pindi wauzapo tumbaku.
Nimetoa wito kwa SSRA waangalie uwezekano wa kuanzisha scheme maalumu ya hifadhi ya jamii kwa wakulima ambapo Serikali ishiriki kwa kuchangia kiwango maalumu katika kila michango ya wakulima. Hii itawezesha wakulima kupata mafao kama bima ya afya, bima ya mazao, mikopo midogo midogo, tofauti za bei na hata elimu kwa watoto wategemezi. Hili ni wazo jipya lakini linapaswa kutazamwa ni kuinua wakulima wa Tanzania. Tusiendelee kuwasahau wakulima. Watanzania wapo Vijijini, tusiwasahau. Umasikini wa Tanzania unaonekana vijijini (rural phenomenon), tutokomeze umasikini kwa kuwekeza kwa mkulima.
Siku ya Tatu: Mpanda Mjini-Ziara Kanda ya Magharibi
Siku ya Tatu: Mpanda Mjini-Ziara Kanda ya Magharibi
Asanteni wananchi wa Mpanda Mjini. Nawashukuru wananchi wa Mkoa wa Katavi. Mapokezi yenu na heshima kubwa mliyonipa mimi na ujumbe wangu imenipa nguvu sana ya kuendelea kufanya siasa za masuala (issues) na majawabu (solutions). Changamoto za maisha magumu vijijini, ardhi, mbolea ya ruzuku, zao la tumbaku na miundombinu tunazibeba na kuwasemea.
Nawapenda sana watu wa Mpanda.
Mungu awabariki.
PICHA
Inyonga, Mpanda Magharibi- Ziara Kanda ya Magharibi
Wananchi wanadhulumiwa kwenye bei ya dola za kimarekani katika kila kilo ya tumbaku ambapo wanapewa bei ya tshs 1400 kwa dola $1 moja! Makato ya pembejeo makubwa na wanashindwa kutoka kwenye umasikini. Tukiwa Sikonge tutatoa kauli kuhusu Wakulima wa Tumbaku na namna ya kuwakomboa.
Tumezugumza umuhimu wa Katiba mpya ya wananchi na namna ya kuepusha mchakato kutekwa na kundi dogo la watu wasiotaka mabadiliko. Tumezungumza kuhusu umuhimu wa mwafaka wa kitaifa katika kuandika katiba ya nchi yetu. Kuweka maslahi ya Taifa mbele ya maslahi ya vyama vya siasa.
Leo tunakwenda Mpanda Magharibi kuanzia Mpanda ndogo mpaka Ikola, Mwambao mwa Ziwa Tanganyika.