Zitto na Demokrasia

Zitto na Demokrasia

Posts Tagged ‘Tanesco

Mapya IPTL: $270Million zimetokaje BoT ?

with 5 comments

Mapya IPTL: $270m zimetokaje BoT ?

THE CITIZEN (Courtesy MillardAyo Blog)

THE CITIZEN
(Courtesy MillardAyo Blog)

THE CITIZEN (Courtesy MIllardAyo Blog)

THE CITIZEN
(Courtesy MIllardAyo Blog)

Nimesoma habari kuu ya gazeti la The Citizen la tarehe 3 Machi 2014 kuhusu mauzo ya kampuni ya IPTL kwa kampuni ya Pan Africa Power Limited (http://www.thecitizen.co.tz/News/-270m-deal–Story-of-IPTL–PAP-and-High-Court/-/1840392/2228606/-/1bddmgz/-/index.html).

THE CITIZEN 4th March 2014 How $270-million IPTL deal was planned and executed

Nimeshtushwa sana na matumizi ya fedha za akiba maalumu (escrow account)  iliyokuwa benki kuu (BoT). Nikiwa mwenyekiti wa kamati ya PAC nina haya ya kusema; Mwaka 2006 Rais Jakaya Kikwete aliagiza kwamba, ili kumaliza kabisa suala la mkataba wa kuuziana Umeme wa IPTL, mitambo ya kampuni hiyo ichukuliwe na Serikali. Mwaka 2006, 2007 na 2008 Kamati ya BUNGE ya Nishati na madini imekuwa ikitoa maagizo hayo hayo kuhusu suala la IPTL. Mwaka 2009, Aprili 30 Kamati ya Bunge ya POAC ilipeleka mapendekezo bungeni kwamba IPTL ichukuliwe na serikali na fedha zilizopo katika escrow account zitumike pia kubadili mtambo ule kutoka mafuta mazito kwenda kutumia Gesi Asilia. Pendekezo hilo lilipitishwa na Bunge na POAC ikatoa maelekezo maalumu kwa Gavana wa Benki Kuu kuwa fedha zilizopo escrow account zisitumike kwa namna yeyote ile bila mitambo ya IPTL kuwa ya umma na kubadilishwa ili itumie Gesi Asilia.

Chanzo cha escrow account?

Baada ya mkataba wa IPTL kuingiwa, iligundulika kuwa kuna udanganyifu mkubwa ulifanyika katika kiwango cha mtaji wa kampuni hiyo na hivyo kufanya malipo wanayolipa tanesco kwa IPTL kuwa makubwa mno. Wakati katika kukokotoa gharama za uwekezaji (capacity charges) mtaji uliowekezwa katika IPTL ulisemwa ni dola milioni 36, ukweli ni kwamba IPTL waliweka dola 50 tu. Hivyo capacity charge ya dola milioni 3 kwa mwezi haikupaswa kulipwa yote kwani kampuni iliendeshwa kwa mkopo kuliko mtaji wa wawekezaji ( debt financed and not equity financed). Hivyo, mahakama ya kimataifa ya ICSID ikaamua kuwa, fedha zote za capacity charges ziwekwe Benki Kuu mpaka gharama halisi ziamuliwe na mahakama ndio wahusika wagawane (tanesco na IPTL). Akiba hiyo, nimeambiwa, ilifika dola 250m kabla ya kuchukuliwa na kugawanywa kwa wanahisa na wanunuzi wa IPTL. Hivyo kabla ya mgawo huu ilipaswa pesa ambazo tanesco walikuwa wanalipa kama ziada ya capacity charges kwa IPTL zirejeshwe kwanza na zinazobakia ndio zilipwe kwa wadai (creditors) na wanahisa. Kwa hali ilivyo sasa mnunuzi wa IPTL kapewa mitambo na fedha za kuinunua, ikiwemo fedha za tanesco ambazo zilipaswa kurejeshwa (Richmond cha mtoto kwa kweli).

Maswali ya kujibiwa ni haya;

Je, ziada ya fedha za malipo ya capacity charges zimerudi tanesco?

Je, mwekezaji Mpya kapewa mkataba Mpya wa kuuza Umeme (PPA) kwa utaratibu gani wa zabuni?

Je, agizo la Rais na BUNGE kwamba Mitambo iwe ya umma limetupiliwa mbali kwa vigezo gani?

Wizara ya Nishati na Madini na Benki Kuu wametoa taarifa rasmi kwa umma kuhusu masuala haya? Wizara itoe taarifa, CAG akague

Kwa namna yeyote ile CAG anapaswa kukagua mchakato huu na kuweka majibu kwa umma kupitia kamati ya PAC. Hii ndio njia bora zaidi ya kuondoa wingu katika suala la IPTL ambalo toka limeanza miaka ya tisini limegubikwa na mazongezonge ya rushwa na uvundo wa kifisadi. Uwazi utatoa ukweli na kuwezesha uwajibikaji wa fedha za umma. Wakati mchakato wa ukaguzi unafanyika ni vema Wizara ya Nishati na madini itoe tamko rasmi.

Zingatia:

Kwa mujibu wa mkataba kati ya TANESCO na IPTL capacity charge inapaswa kukokotolewa kwa kuzingatia mtaji wa asilimia 30 na mkopo wa asilimia 22.31. Mtaji wa IPTL ulikuwa $50 tu, tofauti na $36 milioni zilizotajwa kwenye mkataba na kuamuliwa na mahakama. Badala ya TANESCO kulipa ‘capacity charge’ ya dola 50,000 kila siku Umeme uzalishwe au la, udanganyifu wa mtaji ulipelekea TANESCO kuwa inalipa dola 100,000 kila siku tangu mwaka 2002. Kuanzia mwaka 2007 fedha hizo zilianza kuwekwa kwenye akaunti maalum (escrow account) BoT.

Written by zittokabwe

March 4, 2014 at 3:51 PM

Obama: Uwazi wa Mikataba, Lumumba

with 5 comments

Rais Barack Obama

Rais Barack Obama

Hatimaye Barack Obama, Rais wa Marekani anatembelea tena bara la Afrika. Hii itakuwa ni mara ya pili Obama kutembelea Bara hili alikotoka baba yake baada ya ziara yake ya kwanza mwaka 2009. Mwaka huo alitembelea Ghana na Misri ilhali mwaka huu anatembelea Senegali, Afrika Kusini na Tanzania. Ziara hiyo itakayoanza tarehe 26 mwezi Juni, itamfikisha Tanzania tarehe 1 Julai na kuondoka siku ya pili yake.

Uchaguzi wa Obama kuwa Rais wa Marekani ulipokolewa kwa shangwe Afrika nzima. Wakati Waziri wa mambo ya nje wa Nigeria alilia kwa furaha, nchi ya Kenya ilitangaza siku ya mapumziko na Rais wa zamani wa Afrika Kusini ndugu Nelson ‘Madiba’ Mandela alisema ‘ushindi wa Obama unawafanya Waafrika wathubutu kuota ndoto (Jarida la The Economist). Hapa Tanzania kulikuwa kuna shamra shamra za kila namna na magazeti yaliweka vichwa vya habari kana kwamba ni Rais wa Tanzania aliyechaguliwa. Waafrika walikuwa na matumaini makubwa sana na bwana Obama. Yamefikiwa?

Ni vema ifahamike kuwa Barack Obama ni Rais wa Marekani na siku zote atalinda maslahi ya Marekani tu. Kuwa na matumaini makubwa kwamba labda yeye angeliweza kuiweka Afrika mbele sana ilikuwa ni kujifurahisha tu nafsi. Maslahi ya Marekani ni ya kipaumbele kuliko kitu kingine chochote kwa Rais Obama. Kwa wengi Obama amekuwa kama amewavunja moyo.

Tanzania inapokea kiongozi wa Taifa kubwa duniani wa pili sasa ndani ya kipindi cha miezi 3 tu. Kwanza alikuja Rais wa China na sasa wiki hii anakuja Rais wa Marekani. Maneno ya mtaani na kwenye mabaraza ya majadiliano ni kwamba viongozi hawa wanakuja kugombea maliasili tulizo nazo kama gesi asilia na madini. Nadhani haya ni maneno ya kusema katika kupiga soga maana kunyonywa kwa rasilimali hakuhitaji Rais wa Marekani aje Tanzania. Makampuni yote makubwa yanayochimba dhahabu hapa nchini ni makampuni ya nje na marais wao hawakuja ili waweze kupata mikataba minono ya kuvuna utajiri wetu.  Katika kitalu namba 2 cha utafutaji wa mafuta na gesi huko Bahari Kuu kampuni ya kimarekani ya ExxonMobil ina ubia na kampuni ya Norway ya StatOil. Kampuni hiyo haikusubiri Rais wa Marekani aje ili wapate mikataba.

Kuna makampuni mengi sana ya kichina yanajenga barabara zetu hapa nchini yakiwa na mikataba minono sana. Kule Mchuchuma na Liganga kuna kampuni ya kichina inajiandaa na uchimbaji wa chuma na makaa ya mawe. Makampuni yote haya hayakusubiri Rais wao aje.

Hoja inayojengwa hapa ni kwamba ujio wa Marais mbalimbali nchini ni ujio wa kujijenga kidiplomasia na wakati mwingine kama sehemu ya kutuma ujumbe Fulani kwa dunia. Nchi inayotembelewa pia inaweza kuona kuwa diplomasia yake inaheshimiwa na mataifa yanayoitembelea.

Hata hivyo hii haiondoi ukweli kwamba Obama anakuja kwa ajili ya maslahi ya nchi yake kama ilivyo kwa wachina walivyokuja. Tumesikia Rais Obama ataambatana na mamia ya wafanyabishara kutoka Marekani kwa ajili ya kupata fursa za kuwekeza nchini. Pia tutasikia matangazo kuhusu msaada wa pili wa Millenium Challenge ambapo Wamarekani wanaendelea kumwaga pesa nchini kusaidia miundombinu lakini pia kushawishi kuungwa mkono na nchi zetu kwenye maamuzi Fulani Fulani jumuiya za kimataifa.

Tumesikia Obama atakwenda kutembelea mitambo ya kampuni ya Symbion. Hii ni mitambo ambayo miaka 4 iliyopita ilipigiwa kelele kuwa ni mitumba na hivyo TANESCO wasiinunue. Hawakununua na badala yake kampuni hiyo ya kimarekani ikainunua, wakaingia  mkataba na TANESCO kuwauzia umeme unaozalishwa na mitambo hiyo hiyo chakavu. Wakati tunasuburi kulipa takribani tshs 105 bilioni kwa Dowans baada ya kutubwaga kwenye kesi, tunasubiri kuona wanasiasa watakaokwenda kumsindikiza Obama kwenye matembezi hayo ya kutembelea mitambo chakavu.

Kampuni kubwa ya kutengeneza mitambo ya kuzalisha umeme ya GE imetangaza kuingia ubia na kampuni ya Symbion kuzalisha umeme nchini. Takribani 400MW zitazalishwa kutoka Mtwara na kuingizwa kwenye gridi ya Taifa. Pia sehemu kubwa ya umeme utakaozalishwa Mtwara tayari umepata soko kwenye kiwanda cha kuzalisha udongo ulaya (simenti) cha bwana Dangote kule Mtwara. Mtendaji Mkuu wa GE bwana Jeff Immelt ametangaza kuwa kampuni yake itauza mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi mingi zaidi Afrika Mashariki kuliko Marekani katika kipindi cha miaka mitatu ijayo. Ni biashara tu!

Nishati naona ni kipaumbele kikubwa sana kwa ziara ya Rais Obama. Kwa nchi kama yetu yenye watu asilimia 21 tu wenye umeme, ni dhahiri kipaumbele hiki watu wengi watakiiunga mkono. Hata hivyo Obama ni lazima asimame kidete kuhakikisha kuwa kampuni za nchini mwake zinazopata miakataba hapa nchini ziweke wazi mikataba hiyo na kulipa kodi inavyostahili. Makampuni ya mafuta kutoka Marekani hayana historia nzuri duniani na hivyo ni lazima tulisisitize mapema kabisa. Uwazi wa mikataba na uwezo wa kupambana na ukwepaji kodi ni muhimu sana katika vita dhidi ya Ufisadi na ubadhirifu.

Rais Obama atambue kuwa iwapo Tanzania ingekuwa inakusanya nusu ya kodi zinazokwepwa na makampuni makubwa yanayotumia mbinu kali, basi tungehitaji misaada ya Marekani na hapa nchini angekuja kama mbia wa kweli na sawa katika dunia. Hivyo ni vema aungane na Waziri Mkuu wa Uingereza kuhakikisha kuwa makampuni makubwa hayatumii ‘tax havens’ kukwepa kodi katika nchi kama Tanzania. Uwazi wa mapato yao na kilicholipwa kwa Serikali ni vema usisitizwe sana na Obama mwenyewe ili makampuni yao yasikie na yaache kupora utajiri wa Afrika kiujanja ujanja.

Patrice Lumumba

Mwisho ni vema kama Rais Obama ataomba radhi kwa ushiriki wa Marekani kwenye mauaji wa Waziri Mkuu wa kwanza wa Kongo Patrice Lumumba. Hivi Tanzania inahangaika zaidi ya uwezo wake kupeleka majeshi huko mashariki ya Kongo kulinda amani. Waafrika wengi tunaamini kuwa mauaji ya Lumumba ilikuwa ni kama laana kwa Taifa lile na hivyo limekuwa ni taifa la vurugu na vita licha ya utajiri mkubwa ulioko nchini humo. Nyaraka za CIA zinaonyesha dhahiri kuwa Rais wa Marekani wa wakati huo Lyndon Johnson aliagiza kuuwawa kwa mwanamapinduzi Patrice Lumumba. Kuwaomba radhi Waafrika na hasa Wakongo kuhusu mauaji ya Lumumba ni jambo litakaloweza kusaidia sana kurejesha amani Kongo.

Karibu Afrika, Karibu Tanzania ndugu Barack Hussein Obama.

Written by zittokabwe

July 1, 2013 at 8:56 AM

PRESS RELEASE: Shilingi Bilioni 86 zaibwa Wizara ya Nishati/TANESCO, Gridi ya Taifa hatarini

with 36 comments

Shilingi bilioni 86 zaibwa Wizara ya Nishati/TANESCO, Gridi ya Taifa hatarini

Gazeti la The East African la Novemba 24 – 30, 2012 limetoa taarifa kwamba jumla ya dola za kimarekani milioni 54 zimegundulika kuibwa na watumishi waandamizi wa Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la TANESCO kupitia manunuzi ya Mafuta ya kuendesha mtambo wa Umeme wa IPTL. Gazeti hili limenukuu taarifa ya ukaguzi kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Tanzania (Controller and Auditor General). Taarifa hiyo inasema kuna kikundi (racket) ambacho kazi yake kubwa ni kujifaidisha binafsi na mpango wa umeme wa dharura kupitia manunuzi ya Mafuta mazito ya IPTL.

Itakumbukwa kwamba toka mwaka 2011 kumekuwa na shinikizo lililotolewa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na Waziri Kivuli wa Nishati na Madini kwamba zabuni za ununuzi wa mafuta ya kuendesha mpango wa umeme wa dharura na mchakato mzima wa manunuzi ya mafuta haya ufanyiwe uchunguzi wa kina (forensic audit).

Katika mkutano wa 3 wa Bunge la Kumi (April 2011) niliuliza swali Bungeni kuhusu kashfa hii ya ununuzi wa mafuta ya kuendesha mtambo wa IPTL na baadaye tarehe 16 Aprili 2011 nilimwomba Spika airuhusu Kamati ya Nishati na Madini kufanya uchunguzi kuhusu kashfa hii. Kamati ya Nishati na Madini chini ya aliyekuwa Mwenyekiti ndugu January Makamba ililitaka Bunge kuazimia kufanyika kwa uchunguzi kuhusu suala hili kwenye Taarifa yake ya mwaka 2011 iliyowasilishwa Bungeni mwezi Aprili mwaka 2012. Waziri Kivuli wa Nishati na Madini ndugu John Mnyika katika Hotuba yake ya Bajeti ya Wizara hiyo mwaka 2011 alipendekeza kufanyika kwa uchunguzi kuhusu kashfa hii pia. Juhudi zote hizo hazikuzaa matunda.

Kipindi hicho kiwango kilichokuwa kinahojiwa kuibwa ni shilingi bilioni 15 tu. Taarifa ya The East African kama walivyonukuu kutoka kwenye taarifa ya CAG inaonyesha fedha zilizoibwa ni shilingi bilioni 86.

Zabuni za kununua mafuta ya kuendesha umeme wa dharura zimekuwa zikitolewa bila kufuata utaratibu wa zabuni kwa mujibu wa Sheria ya manunuzi. Hivi sasa kila mwezi Tanzania inatumia dola milioni 70 kununua mafuta ya kuendesha mitambo ya umeme. Fedha hizi zinatoka Hazina na sehemu ndogo kutoka TANESCO. Wakati fedha hizi bilioni 112 zinachomwa kila mwezi kununua mafuta mazito na dizeli ya kuendesha mitambo ya umeme, Taarifa za kitaalamu zinaonyesha kwamba Bwawa la Mtera hivi lina kina cha maji chini ya kiwango kinachotakiwa na uzalishaji wa umeme ni asilimia 20 tu ya uwezo (installed capacity). Iwapo TANESCO wataendelea kutumia zaidi maji yaliyopo Mtera, Mitambo itashindwa kazi na Gridi nzima itasimama maana Mtera ndio nguzo kuu ya Gridi ya Taifa. Hali hii ni hatari sana kwa uchumi na ulinzi na usalama wa Taifa. Kimsingi Gridi ya Taifa ipo hatarini kutokana na kiwango cha Maji kilichopo Mtera hivi sasa na kuendelea kupungua kwa kina hicho cha maji.

Wananchi wanapaswa kuelezwa kinaga ubaga nini kinaendelea katika sekta ndogo ya umeme hapa nchini;

1.      Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kuhusu zabuni za manunuzi ya Mafuta ya kuendesha mitambo ya umeme wa dharura iwekwe wazi na ‘racket’ inayosemekana kuiba jumla ya shilingi bilioni 86 ionyeshwe na hatua za kisheria zichukuliwe mara moja na bila kuchelewa.

2.      Waziri wa Nishati na Maadini auleze umma hali yalisi ya sekta ya umeme nchini, uzalishaji wa umeme upoje, hali ya maji katika bwawa mkakati la Mtera na nini hatma ya mitambo ya IPTL, kesi zake na utekelezaji wa mapendekezo ya Bunge kuwa kesi za kampuni hii zimalizwe nje ya mahakama. Pia Taifa lielezwe Mpango wa Dharura wa umeme unakwisha lini maana muda uliotolewa na Bunge mwezi Agosti mwaka 2011 tayari umekamilika. Waziri aeleze hatua agni amechukua baada ya kukabidhiwa taarifa na CAG kuhusu maafisa waandamizi wa Wizara waliohusika na wizi wa shilingi bilioni 86 za kununua mafuta ya IPTL.

3.      Waziri wa Fedha na Uchumi aueleze umma ni kiwango gani cha fedha Hazina imetoa kununua mafuta ya kuendesha mitambo ya umeme wa dharura kati ya Mwezi Novemba mwaka 2011 na Oktoba mwaka 2012 na kama taratibu zote za zabuni zilifuatwa na pale ambapo hazikufuatwa ni hatua gani PPRA wamechukua dhidi ya waliokiuka sheria ya manunuzi na kuleta hasara ya mabilioni ya fedha kwa Serikali.

 

Kabwe Zuberi Zitto, Mb

Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Waziri Kivuli wa Fedha

Dar es Salaam. Novemba 25, 2012

Kigoma Kaskazini – a Potential Kerosene Free Constituency?

with 2 comments

Parliamentarians perform three core duties – Legislating, representation and oversight.

Ironically, one key duty is not constitutional – constituency promotion. Increasingly in Tanzania a Member of Parliament is judged not on his constitutional duties, but on constituency promotion duties like bringing in development projects such as roads, water, schools, hospitals and medicine etc. to the constituency, creating jobs and by making a lot of noise in Dodoma.

The people of Kigoma Kaskazini credit my service to them through several fronts but two that stand out is the road construction (the 60KM tarmac road Mwandiga-Manyovu & 34KM Kigoma-Kidahwe) and the other my being very vocal in Parliament. During my re-election campaign in 2010 my constituents in various meetings time and again reiterated the following “roads are done; now we want electricity”. True to their word they have been very vocal and holding me to account especially the coffee farmers of Kalinzi who want to add value to their coffee and get a better return.

The umeme vijijini is not an easy agenda and it is tough getting rural electrification projects from Rural Energy Agency (REA) as costs are very high and the government always gives them a small budget. In the 2011/2012 Budget about TZS 6.5bn was allocated to power 12 villages in Kigoma Kaskazini, but not one single shilling has been remitted to REA from the central government to implement the project. Rural electrification has remained a favorite catch phrase from the government and politicians to wananchi and usually elicits a lot of emotion but we have little to show as progress.

Kigoma Region, mainly Kigoma Town, uses diesel-powered thermal generators with installed capacity of 11MW. However, only 3-4MW is being produced – the cost of producing power in Kigoma is very high. While TANESCO spend TZS 1bn monthly to run Kigoma Generators, it collects about TZS 133Million.

Spurred by this and the many challenges that Kigoma has as a region and my constituency are facing, and being a green energy advocate, I have been championing for a green project working with a US based company known as KMR Infrastructure on a biomass project to produce 10MW of electricity in Kigoma and shut off expensive diesel generators.

The other day I had the opportunity and pleasure to meet the CEO of KMRI here in Washington DC and we discussed a number of issues with regard to their biomass project and other green projects/initiatives that I felt I should share. Some of the highlights from my meeting were;

  • By displacing TANESCO diesel mini-grids with biomass power it reduces TANESCO operating costs by 45%, generates thousands of local jobs in agriculture and uses local agricultural biofuel supply to displace imported diesel creating longer sustainable benefits to the region
  • Up to 25 Million USD will be invested into this biomass power plant in Kigoma over the coming 3 years.
  • In this project 1000 families will be provided with 5 hectares of land each for a bamboo plantation and bamboo will provide fuel for power generation. More jobs will be created through the whole value chain including transportation services. With strong linkages to the rural economy, the project is expected to have enormous positive effects to the people of the Region.
  • Power will increase in Kigoma, jobs created and TANESCO will cut their costs.

 

Kerosene Free Constituency

How will this alternative power solution transform the lives of people from low-income househoulds? KMRI had an answer that I coined “a kerosene free constituency” as highlighted below;

Most of Tanzanian villages’ households use kerosene or paraffin lamps for lighting. By setting up centralized solar charging stations, we could make entire villages kerosene free by replacing oil wick lamps with battery powered CFL light. This will reduce monthly lighting bill by 50% for rural households, provide 40 times better lighting and avoid health hazards from using kerosene or paraffin lighting.

The central village charging centers also act as employment opportunity for rural entrepreneurs providing them USD 3-4 per day in income and also creating immediate market based sustainable electrification program for Tanzanian villages.

Leveraging the proposed renewable biomass plant in Kigoma, a distributed renewable energy infrastructure would be setup to make this kerosene free village initiative.

As a starting point the biomass plan will help 20-40 entrepreneurs set up central solar charging stations in villages and charge 50-100 battery powered CFL lamps. The charging centers will use solar power during the day to charge CFL lights and then sell to households charged lamps that provide 15-20 hours of lighting. After the battery is exhausted, the households return the empty battery lights and can buy another charged light for fresh usage, similar to buying additional kerosene for their lamps. This pay per use model is similar to their current buying patterns and so will be easier to adopt as it is in line with existing habits.’

The daily cost of these CFLs will be 50% less than using kerosene for similar hours in a day.

The CFLs apart from being cheaper will provide considerably much better lighting and hence reduce strain on eyes.

Displacing kerosene also has other benefits like avoiding indoor smoke pollution, eye irritation and fire hazards.

In addition to lighting, the central solar station can also be used to charge cell phone batteries avoiding expensive trips to town and cutting cell phone charging costs by more than half. Providing a reliable and cheap source of charging a phone removes a huge constraint in mobile adoption thus promoting more telecommunication usage in rural areas, leading to increased economic activity, banking services, information availability, and reduced travel time.

The biomass power plant provides the necessary centralized infrastructure to equip and train the entrepreneurs, provide technicians to provide ready technical and operational support to the charging stations to ensure their continued successful functioning”.

Kigoma will also benefit from MCC funded project on solar power.

The solar project will put solar power on “45 secondary schools, 10 health centres, 120 dispensaries, municipal buildings and businesses across 25 village market centres currently without access to the electricity grid.

Camco International, a global clean energy developer, and Rex Investment Limited (RIL), a solar power contractor based in Tanzania, were just awarded USD 4.7 million for this rural Tanzanian solar power project in the region of Kigoma. Source: Clean Technica.

I am not just dreaming of seeing a Mwamgongo village woman throwing away a koroboi and embracing a cleaner energy at lower costs than kerosene, that costs much more in Kigoma, and in Mwamgongo in particular, compared to other places in Tanzania. Kerosene- free villages are in sight. A ‘koroboi’ free Kigoma Kaskazini is possible.

Hard work and focus are necessary. Going beyond the constitutional duties of a member of Parliament is necessary to transform the lives of our people.

Written by zittokabwe

May 17, 2012 at 1:49 PM