Posts Tagged ‘CAG’
Tamko la Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo ndg. Zitto Kabwe kuhusu Ripoti ya CAG mwaka 2013/2014
Tamko la Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo ndg. Zitto Kabwe kuhusu Ripoti ya CAG mwaka 2013/2014
1) Taarifa nyingine ya CAG imetoka, kwa mujibu wa Katiba ya JMT na kwa mujibu wa sheria za nchi. Taarifa hii imechelewa kutolewa kulingana na mabadiliko ya Ratiba za Bunge ambapo hapo awali taarifa ilikuwa ikitoka mwezi Aprili na kuwezesha kuchangia katika mchakato wa Bajeti ya nchi. Taarifa ya mwaka huu na ile ya mwaka Jana imetoka wakati wa Bunge la Bajeti na hivyo Bajeti ya Serikali haijazingatia hoja za ukaguzi ili kuboresha mfumo wa matumizi ya fedha za umma. Ni vema utaratibu wa zamani wa ripoti kutolewa mwezi Aprili urejewe ili wabunge waweze kutumia ripoti hizo wakati wa kamati katika kujadili makadirio ya Bajeti za Wizara mbalimbali.
2) Taarifa kama miaka iliyopita bado sio nzuri. Mapato mengi ya Serikali bado yanapotea. Uk. 53 wa Taarifa unaonyesha kuwa mizigo inayoingizwa nchini kupita kwenda nchi jirani zinazotumia bandari zetu hubakia nchini na kuingizwa sokoni hivyo kukwepa kodi. Mwaka 2013/2014 mizigo ya transit iliyobaki nchini kiudanganyifu ilikuwa zaidi ya bidhaa 6000 kwa mujibu wa Taarifa ya CAG. Hivyo kodi ya tshs 836 bilioni haikulipwa kwa mizigo hiyo sawa sawa na 10% ya makusanyo yote ya kodi za ndani. Tshs 836 bilioni ilipotea mwaka 2013/14 peke yake. Wakati hili linatokea Serikali ipo ukata mkubwa na kushindwa kuendesha miradi yake mbalimbali. Fedha iliyokwepwa idara ya forodha peke yake inalipa Madeni yote ya wakandarasi wa barabara wanaoidai TANROADS na riba kulimbikizwa kila mwaka. Fedha hii ingelipa Madeni yote ya mfuko wa PSPF wanayoidai Serikali. Fedha hizi zingeweza kulipia miradi 2 mikubwa nchini ya BVR na vitambulisho vya Taifa ambayo inasuasua kutokana na ukata.
Natoa wito kwa CAG kwanza kuweka wazi orodha ya bidhaa hizo zilizobakia nchini na kuingizwa nchini bila kulipa kodi. Vile vile CAG aweke wazi wafanyabiashara wote walioagiza bidhaa hizi na vyombo vya kiuchunguzi vichukue hatua za kuwashtaki wafanya biashara hawa mara moja.
Natoa wito kwa Kamati ya Bunge ya PAC kuwaita mara moja maafisa wa TRA kujieleza mbele ya kamati kuhusu suala hili na kuandaa taarifa maalumu bungeni ili kuanika uoza huu unaopoteza mapato mengi sana ya Serikali.
3) CAG kaonyesha kuwa kuna ubadhirifu mkubwa sana kitengo cha maafa cha ofisi ya Waziri Mkuu ambapo tshs 163 billioni za chakula cha maafa hazikukusanywa katika kipindi cha miaka 5 iliyopita. Huu ni kama mrija wenye wastani wa tshs 32 bilioni kuchotwa kwa kisingizio cha chakula cha maafa kwa wananchi. Kwa malezo ya CAG ni kwamba Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wamekula fedha za chakula cha misaada. Maana hakuna uthibitisho wa kuwa mahindi yaliyogawanywa na taarifa kutolewa na Wakala wa Akiba ya Chakula (NFRA). Kitengo cha maafa ofisi ya PM kimekuwa mrija wa wizi wa fedha za umma, wizi ambao umekuwa ukifanyika bila ya kugunduliwa kwa miaka 5 sasa. ACT Wazalendo inaisihi Kamati ya Bunge ya PAC kufanya uchunguzi maalumu kwenye kashfa hii ya tshs 163 bilioni katika Ofisi ya Waziri Mkuu na Wakala wa Hifadhi ya Chakula ( NFRA).
4) ACT Wazalendo inalitaka Bunge kuchukua stahiki dhidi ya Wizara ya Ujenzi kufuatia ripoti ya CAG kuonyesha kuwa Wizara ilidanganya Bunge katika kupitisha Bajeti ya tshs 252 bilioni ambapo kati yake tshs 87 bilioni ziliibiwa au matumizi yake kutoeleweka.
5) ACT Wazalendo inampongeza CAG kwa kuendelea na zoezi la kisheria la kukagua mahesabu ya vyama vya siasa. Hii inaweka misingi ya uwajibikaji kuanzia kwenye vyama vya siasa, taasisi muhimu sana katika ujenzi wa demokrasia. Vyama vya siasa vichukulie ripoti ya CAG kama changamoto ya kutoa kwanza kibanzi kwenye macho yao ili kuwa na ‘ moral standing’ ya kupambana dhidi ya ubadhirifu wa fedha za umma nchini.
Zitto Kabwe
Kiongozi wa Chama ACT Wazalendo
RATIBA -KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC) JANUARI 2015
KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC)
RASIMU YA RATIBA YA UKAGUZI WA MIRADI NA KUJADILI HESABU ZILIZOKAGULIWA ZA SERIKALI KUU NA MASHIRIKA YA UMMA KUANZIA TAREHE 05 HADI 24 JANUARI 2015,
MKOA WA MOROGORO NA OFISI NDOGO YA BUNGE, DAR ES SALAAM
Ukaguzi Maalumu akaunti ya Tegeta Escrow-Hadidu Rejea-PAC
Ukaguzi Maalumu akaunti ya Tegeta Escrow
Hadidu rejea
1) Kuchunguza uendeshaji wa mkataba wa kuzalisha Umeme kati ya kampuni ya IPTL na TANESCO
2) Kuchunguza kama wakati escrow inafunguliwa kampuni ya mechmar ilikuwa inamiliki IPTL, kama ilikuwa imefilisiwa na kama ilikuwa imehamisha umiliki wake kwa kampuni ya PAP.
3) Kuchunguza na kuthibitisha ushahidi wa kampuni ya PAP kununua kampuni ya mechmar na kumiliki IPTL
4) Kuchunguza chanzo cha mgogoro kuhusu tozo kati ya TANESCO na IPTL na kuthibitisha ushahidi wowote kuwa mgogoro uliamuliwa kwa faida ya IPTL
5) Kuchunguza kama ilikuwa sahihi kwa mwanasheria mkuu wa Serikali kusamehe kodi ya VAT ya jumla ya tshs 26 bilioni kutokana na tozo ya capacity charges na TRA wachukue hatua gani kuhakikisha kodi hiyo inakusanywa
6) Kuchunguza kiwango cha fedha kilichopaswa kuwemo katika akaunti ya escrow, kiwango gani kilikuwepo wakati IPTL wanalipwa na kiwango gani kitapaswa kulipwa zaidi kutoka tanesco
7) Kuchunguza madai ya benki ya standard chartered kwa tanesco na madai mengine yeyote yanayohusiana na mkataba wa kuzalisha Umeme wa IPTL na iwapo Serikali imejihadhari na uwezekano wa madai yanayoweza kufunguliwa, nafasi na heshima ya nchi katika kuheshimu mikataba ya kimataifa na ya uwekezaji.
8) Kuchunguza iwapo Wizara ya Nishati na madini ambayo ni mhusika Mkuu wa akaunti ya tegeta escrow ilifanya ‘due diligence’ ya kutosha kabla ya kuingia makubaliano ya kutoa fedha zilizopo akaunti ya tegeta escrow. Kupata Maelezo ya Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na madini ni kwa nini aliagiza ukaguzi maalum wakati yeye ni mhusika Mkuu kwenye mchakato mzima na ilhali akijua PAC tayari imeanza mchakato wa ukaguzi.
9) Kutoa mapendekezo ya njia bora za kisheria kulinda Taifa kutoingia hasara zaidi katika mkataba wa IPTL chini ya wamiliki wapya
10) Kutoa ushauri kwa kamati ya PAC juu ya mapendekezo ya hatua ambazo Bunge linapaswa kuchukua kuhusu matokeo ya ukaguzi huu maalumu
Imetolewa na;
KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC)
CAG yet to receive parties audit reports
CAG yet to receive parties audit reports
Chairman of the Parliamentary Public Accounts Committee (PAC),Mr Zitto Kabwe PHOTO|FILE
In Summary
NCCR-Mageuzi chairman James Mbatia refuted reports that the party has not submitted its audit reports for four consecutive years.
Dar es Salaam. The office of the Controller and Auditor General (CAG) said yesterday it was yet to receive audit reports from any of the nine political parties getting subvention.
The remark is in response to a controversy triggered by remarks of the chairman of the Parliamentary Public Accounts Committee (PAC), Mr Zitto Kabwe. His committee has since summoned six of the parties to explain why their accounts were yet to be audited.
The response by the deputy CAG, Mr Francis Mwakapalila, is likely to intensify the subvention controversy which has put the political parties and Mr Kabwe in a face-off in the last one week.
Zitto has accused nine political parties with representation in the Parliament of failing to submit their financial accounts to the CAG for auditing. He directed the registrar of political parties to suspend the subsidies of the parties for their failure to comply with the guiding law.
Zitto claimed that the parties had failed to submit audit reports accounting for a total of Sh67.7 billion in the past four years — a requirement made by the Political Parties (Amendment) Act, 2009.
The deputy CAG told The Citizen that the truth about the controversy will be known on Friday at a joint meeting of all the parties.
He, however, clarified that the CAG’s office had allowed parties to seek the services of external auditors. According to Mr Mwakapalila, the CAG can contract qualified firms to audit the political parties.
“Political parties are expected to maintain proper accounts every year and submit their financial reports, audited by the CAG, to the registrar of political parties,” he detailed.
PAC has summoned the parties on Friday to explain why they failed to submit the said reports. “We will know who was right or wrong, I hope the CAG will also be there. Let’s be patient,” he added.
The nine political parties have been insisting that they have submitted their audited accounts to the CAG and accused Mr Kabwe of overstepping his mandate.
Already, the Civic United Front (CUF) said it would not attend the Friday meeting and accused Mr Kabwe of acting beyond his legal powers.
The party’s deputy secretary general (Mainland), Mr Julius Mtatiro, said his party was not on the list of the parties that have not submitted their audit reports.
The ruling CCM has strongly accused the PAC, saying it was aware of the requirements of the law and that the it had has been submitting its audit reports to the CAG.
Its Publicity and Ideology secretary, Mr Nape Nnauye, said the Tanzania Audit Corporation has audited its accounts from 2003/04 to 2010/2011. “We’re waiting for the 2011/2012 audit report which is still with the external auditors,’’ adding that the report would be forwarded with the CAG once it is ready.
NCCR-Mageuzi chairman James Mbatia refuted reports that the party has not submitted its audit reports for four consecutive years.
“Our accounts were audited and we sent reports to the registrar,’’ he said.
He said, however, that the CAG’s office was cash-strapped and unable to oversee the auditing of political parties.
Chadema Information officer, Mr Tumaini Makene, said his party was playing by the rules as far as financial propriety and transparency were concerned. According to Zitto’s committee, CCM has failed to account for Sh50.97 billion, Chadema (Sh9.2 billion), CUF (Sh6.29 billion), NCCR-Mageuzi (Sh677 million), UDP (Sh33 million), TLP (Sh217million), APPT-Maendeleo (Sh11 million), DP (Sh3.3 million) and Chausta (Sh2.4 million).
Meanwhile, two PAC members yesterday defended Mr Kabwe against attacks by political parties allegedly for personalising the subvention issue, saying the matter was owned by the Committee.
They told The Citizen separately that Zitto had full blessings of members of the PAC before he made the statement to the effect that accounts of nine political parties had not been audited for four years.
“That is the position of our committee and not Zitto’s creations as political parties want the public to believe,” said a member of the committee, Mr Abdul Marombwa.
He said they were wondering why the political parties were personalising the issue while the matter surfaced the committee met registrar of political parties, Mr Francis Mutungi, who revealed the information.
“There is no Zitto’s agenda here, we all sat and agreed on the matter,” he said.
Another PAC member who asked not be named said their team was implementing Political Parties (Amendment) Act, 2009, which requires them to submit the parties accounts to the CAG for auditing and forward the audit reports to the registrar.
“The registrar confirmed to us none of the nine parties fulfilled that legal requirement,” he said.
“That was not Zitto’s statement, it was the outcome of the meeting,” he insisted.
Source: THE CITIZEN http://www.thecitizen.co.tz/News/Cag-yet-to-receive-parties-audit-reports/-/1840392/2041932/-/jwtkmj/-/index.html
RUZUKU YA VYAMA VYA SIASA
Shilingi bilioni 67.7 zimelipwa na Serikali kwa vyama vya siasa katika kipindi cha miaka 4, 2009/2010 mpaka 2012/2013. Fedha hizi hazijakaguliwa kwa mujibu wa Sheria.
Mahesabu ya Vyama vya siasa nchini yanapaswa kukaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali kwa mujibu wa Sheria tangu mwaka 2009. Tangu mwaka huo Kamati ya PAC haijawahi kuona Taarifa ya CAG kuhusu ukaguzi wa vyama vya siasa. Nilihoji tangia Aprili 2011 https://zittokabwe.wordpress.com/category/ruzuku-vyama-vya-siasa/
Kamati imemwita Msajili wa vyama ili kufafanua ni kwa nini Vyama vya Siasa nchini havifuati sheria (vifungu vya sheria vimeambatanishwa hapa chini). Uvunjifu huu wa Sheria ni wa makusudi au wa kutokujua? Sheria inataka Mahesabu ya vyama yatangazwe kwa uwazi, tena kwa Government Notice. Umewahi kuona? Tarehe 15 Oktoba, 2013 Kamati ya PAC itatafuta majibu haya kutoka kwa Msajili na ikibidi vyama vyenyewe. Tunataka uwazi wa matumizi ya Fedha za Umma.Vyama vya siasa ndio vinaunda Serikali, uwazi unaanzia huko ili kuepuka fedha chafu kama za EPA kuingia kuvuruga uchaguzi.
Vyama vifuatavyo vimepokea Ruzuku ya jumla shilingi bilioni 67.7 tangu mwaka wa fedha 2009/2010;
- CCM tshs 50.97 bilioni
- CHADEMA tshs 9.2 bilioni
- CUF tshs 6.29 bilioni
- NCCR – M tshs 0.677 bilioni
- UDP tshs 0.33 bilioni
- TLP tshs 0.217 bilioni
- APPT – M tshs 11 milioni
- DP tshs 3.3 milioni
- CHAUSTA tshs 2.4 milioni
Political Parties Act, No. 5 of 1992 as ammended from time to time.
14. -(1) Every political party which has been fully registered shall—
a) maintain proper accounts of the funds and property of the party;
b) submit to the Registrar –
“(i) an annual statement of the account of the political party audited by the Controller and Auditor-General and the report of the account.” (This became law in March, 2009)
ii) an annual declaration of all the property owned by the party.
(2) The Registrar, after inspecting any accounts or report submitted pursuant to this section may, for the benefit of the members or the public, publish any matter relation to the funds, resources or property of any party or the use of such funds, resources or property.
(3) The Registrar shall publish in the official Gazette, an annual report on the audited accounts of every party.
18. -(1) Subventions granted to a party may be spent only on
(a) the parliamentary activities of a party;
(b) the civil activities of a party;
(c) any lawful activity relating to an election in which a party nominates acandidate;
(d) any other necessary or reasonable requirement of a party.
(2) Subventions granted to a political party shall be accounted for to the Registrar, separately from the accounting for other funds of the party.
(3) Any party which fails or neglects to account for subventions in accordance with this Act, shall forfeit the right to any subsequent subvention due to the party in accordance with this Act.
(4) Where the Registrar is for any reasonable cause, dissatisfied with any account of subventions submitted by any party, so much of the subvention which has not been accounted for or has not been accounted for satisfactorily, shall be deducted form any subsequent subvention due to the party.
(5) If by reason of failure to submit an account or for any other reason, the Registrar has reason to suspect that any offence under the Penal Code may have been committed in relation to the money which has not been committed in relation to the money which has not be been accounted for, he may make a report to a police station, and the officer in charge of that police station shall cause the matter to be investigated.
18A. Notwithstanding the provisions of sections 14 and 18, every political party receiving subvention in accordance with this Act shall, not later than 3151
October every year, submit to the Registrar financial statements and audited accounts reflecting any other source of funds and details regarding the manner in which such funds were used.” (became law in 2009)
HATI ZA KUMILIKI ARDHI ZITOLEWE UPYA, ZA DIJITALI NA ZIHUSISHWE NA NAMBA YA MLIPA KODI (TIN)
HATI ZA KUMILIKI ARDHI ZITOLEWE UPYA, ZA DIJITALI NA ZIHUSISHWE NA NAMBA YA MLIPA KODI (TIN)
Kamati ya Hesabu za Serikali imekutana na Wizara ya Ardhi kwa madhumuni ya kupitia Hesabu za Wizara kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 2012. Changamoto za Wizara ni nyingi sana na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) amehoji mambo mengi sana na mengi ni wizi, upotevu wa mapato ya Serikali na malalamiko ya wananchi kuhusu ardhi. CAG alitoa hoja za ukaguzi maeneo ya mapato kutokusanywa, kulimbikizwa na hata kukusanywa bila kuyawasilisha Wizarani.
Katika Mwaka wa Fedha 2011/12 Wizara ilipangiwa kukusanya jumla ya Shilingi bilioni tisini na tisa (99 bilioni) lakini ilikusanya shilingi bilioni ishirini tu (20 bilioni) sawa na asilimia 21 ya makadirio.
CAG pia alihoji masuala ya viwanja vilivyopimwa, kugawiwa watu lakini watu hawakupewa hati ambapo zaidi ya viwanja 7, 342 vilikutwa ni viwanja vyenye shaka. Pia viwanja 160 jijini Dar es Salaam vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 555.8 milioni viligundulika ni viwanja ambavyo walijigawiwa maafisa wa Ardhi maana haoakuwa na ushahidi wowote wa mauzo ya viwanja hivyo. Hoja nyingine ni pamoja na ukiukaji wa sheria kwa kujengwa kwenye fukwe nk.
Katika Ripoti ya Hesabu za Serikali Kuu 2011/12 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali alipendekeza kuanzishwa kwa haraka mfumo fungamanifu wa Taarifa za Ardhi, kutunza kumbukumbu kielektroniki na kuunganisha kuanzisha utaratibu wa kwamba wakati wa kusajili hati ya ardhi anayesajili kuwa na namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN).
Baada ya mjadala wa kina na kushauriana na wakaguzi na wataalamu Kamati ya Hesabu za Serikali iliona kuwa kuna haja kubwa sana ya kufanya mabadiliko makubwa kwenye mfumo mzima wa kutoa hati za kumiliki Ardhi. Hivyo Uamuzi mkubwa tuliochukua ni kuagiza kuwa hati zote za kumiliki ardhi zitolewe upya, ziwe za dijitali na hati ziendane na namba ya Mlipa kodi (TIN).
Kamati imeagiza kuwa Wizara kutoa majibu ya utekelezaji wa agizo hilo ifikapo Mwezi Januari mwaka 2014. Tunaamini kuwa iwapo hati zote za ardhi zitakuwa za dijitali, tutaondoa kabisa tatizo la hati mbili kwenye kiwanja au shamba moja, itakuwa ni rahisi kwa usimamizi wa ardhi na itaondoa mgogoro mingi ya ardhi hapa nchini. Pia tunadhani pia itakuwa rahisi kujua nani anamiliki ardhi kiasi gani, wapi nk.
Tunaamini kuwa mfumo wa dijitali katika hati za ardhi utaongeza usalama zaidi kwa wamiliki wadogo wa ardhi na kuondokana kabisa au kwa kiasi kikubwa na hati za bandia ambazo zinaumiza zaidi wananchi masikini wanaotapeliwa kila wakati. Ardhi yenye hati za kidijitali na zinazotunzwa kielektroniki zitakuwa na thamani zaidi na zitawezesha mahitaji zaidi ya hati hizo kwa shughuli mbalimbali za wananchi.
Mapato yatokanayo na umiliki yatakusanywa kirahisi sana na kwa kuwa kila hati itakuwa na namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN) itakuwa ni njia rahisi ya kuzuia ukwepaji kodi ya ardhi. Kwa kuwa kamati imeagiza kuanza kutumika kwa risiti za elektroniki kwa malipo ya serikali, tutaweza kupandisha mapato ya Serikali na hasa kwenye halmashauri za wilaya na kuepukana na kodi sumbufu kwa wananchi.
Changamoto kubwa ni kama matajiri wenye ardhi kubwa watakubali mageuzi haya kwani hawapendi ijulikane kiwango cha ardhi wanachomiliki na pia itazuia ukwepaji kodi na kupunguza rushwa kwa watendaji wa Wizara ya Ardhi.
Mfumo huu hata hivyo uwezeshe watu kuweza kutafuta kwenye mtandao hati, iwe rahisi kutafanya utafutaji. Pia mfumo huu unaweza kusaidia sana suala la fidia kwa wananchi wanaohamishwa kupisha uwekezaji mkubwa kama kwenye sekta za madini na gesi asilia. Kwa mfano mwekezaji atapaswa kuhakikisha hati za kijiditali zinapatikana kwa wananchi wanaohamishwa kupisha mradi baada ya maridhiano ya wananchi hao kuhusu kupisha mradi na mahala watakapohamia.
Kuna haja pia hata hati za madini (mining rights) na leseni mbalimbali ziwe za dijitali na kuhusishwa na TIN. Huko ndipo tunapaswa kuelekea.
Zi
Zitto Kabwe
MwenyeKiti PAC
Agosti 21, 2013 – Dar es Salaam
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Shilingi bilioni 620 za Deni la Taifa hazina maelezo
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Shilingi bilioni 620 za Deni la Taifa hazina maelezo
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ametoa taarifa yake ya mwaka 2011/2012 na kuonyesha kuwa kuna skandali kubwa sana katika akaunti ya Deni la Taifa. Nanukuu
‘Uhakiki wa mchanganuo wa madeni ya Taifa kama ulivyokuwa tarehe 30 Juni, 2012 ulibaini kuwepo kwa marekebisho ya deni ya shilingi 619,803,554,183.91 ambayo uongozi haukuweza kutoa maelezo ya kuridhisha.’ (Taarifa ya CAG, Ripoti ya Serikali Kuu 2011/2012 uk 158). Mwisho wa Kunukuu
Katika Taarifa yake hiyo CAG anaendelea kuonyesha kuwa Deni la Taifa linazidi kukua na mwaka unaoishia mwezi Juni 2012 deni lilikuwa kwa asilimia 17 kutoka mwaka unaoishia mwezi Juni 2011.
Kukosekana kwa maelezo ya kuridhisha kuhusu zaidi ya nusu trilioni za Deni la Taifa ni jambo linalopaswa kutiliwa mashaka makubwa, kuchunguzwa na kupata majawabu stahiki. Tafiti mbalimbali duniani zinaonyesha kuwa kuna mahusiano makubwa sana kati ya Deni la Taifa la utoroshaji wa fedha kwenda kwenye mabenki ya ‘offshore’. Katika kitabu cha ‘Africa’s Odious Debts: How Foreign Loans and Capital flight bled a continent’ kilichoandikwa mabwana Leonce Ndikumana na James Boyce imeonekana kwamba Deni la Taifa huchochea utoroshwaji wa Fedha kwenda kuficha nje ya Tanzania.
Mabilioni haya kwenye akaunti ya Deni la Taifa yanashtusha sana. Kambi ya Upinzani Bungeni kwa miaka miwili mfululizo imekuwa ikitaka ukaguzi maalumu kwenye akaunti za Deni la Taifa lakini Serikali imeshindwa kufanya hivyo. Nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya PAC pia nimemtaka CAG afanye ukaguzi huu maalumu.
Kambi ya upinzani Bungeni ilisema hivi katika Bajeti yake kivuli 2012/13:
DENI LA TAIFA
Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inasikitika kwa serikali kuendelea kutengeneza madeni kwa Taifa kwa kuendelea kukopa zaidi kwa matumizi ya kawaida ya serikali. Wakati Serikali inasisitiza kwamba Deni letu linastahmilika, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali anaonyesha mashaka makubwa sana kutokana na kasi ya kukua kwa Deni la Taifa. Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inaonyesha kuwa Deni la Taifa linazidi kuongezeka kwa asilimia 38% kutoka shilingi trillion 10.5 mwaka 2009/2010 hadi shilingi trillion 14.4 mwaka 2010/2011. Kwa mujibu wa Waziri wa Fedha Deni la Taifa limefikia shilingi trillion 20.3 mpaka ilipofika mwezi Machi mwaka 2012. Ukisoma taarifa ya Mwezi wa Mei 2012 ya Benki Kuu ya Tanzania, Deni la Taifa sasa limefikia shilingi trillion 22.
Mheshimiwa Spika, Suala hapa sio ustahmilivu wa Deni kama inavyodai Serikali bali ni kwamba tunakopa kufanyia nini? Bajeti ya Mwaka 2012/13 inayopendekezwa inaonyesha kwamba Serikali itakusanya shilingi trilioni 8.7 kama makusanyo ya ndani na itatumia shilingi trilioni 10.6 kama matumizi ya kawaida. Ni dhahiri kwamba sehemu ya mikopo ambayo serikali inachukua sasa itakwenda kwenye matumizi ya kawaida. Hatutaki mikopo kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya posho, kusafiri, magari nk. Tuchukue mikopo kuwekeza kwenye miradi itakayokuza uchumi na kuzalisha kodi zaidi. Bajeti inaonyesha kwamba Serikali itakopa shilingi takribani trillion 5 mwaka 2012/13. Serikali ikubalikutekeleza mapendekezoya Kambi ya Upinzani ya kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kupanua wigo wa kodi katika maeneo muhimu kama sekta ya madini na mawasiliano, kuzuia misamaha ya kodi, kutokomeza ukwepaji kodi, na kuepuka matumizi mabaya ili kuepuka madeni yasiyo ya lazima.
Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inapenda kusisitiza kwamba Bunge lifanye ukaguzi maalumu kuhusu akaunti ya Deni la Taifa ili kuweza kubaini ukweli kuhusu ustahmilivu wa Deni na mikopo ambayo Serikali inachukua kama inakwenda kwenye Maendeleo na miradi ipi na kama miradi hiyo ina tija. Vilevile tumependekeza kwamba Mikopo yote ambayo Serikali inachukua iwe inapata idhini ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi au Bunge litunge sharia ili kiwango cha juu cha kukopa ambacho Serikali haipaswi kuvuka. Kuiacha Serikali inaendelea kukopa bila mpango ni kuliweka Taifa rehani na kupeleka mzigo wa kulipa madeni haya kwa kizazi kijacho. Hatuwezi kukubali Wazee wetu waishi maisha yao, waishi maisha yetu na pia wakope maisha ya watoto wetu. Mwisho wa kunukuu.
Kambi ya Upinzani inarejea kutaka ukaguzi maalumu kuhusu akaunti za Deni la Taifa na maelezo ya kina ya Serikali kuhusu shilingi 620 bilioni ambazo hazina maelezo kwenye Deni la Taifa. Hatuwezi kukaa kimya kuona Watanzania wanabebeshwa madeni ambayo kimsingi ni madeni bandia yanayotajirisha watu wachache wenye uwezo na ujasiri mkubwa wa kuiba, kupora nakufisidi hazina ya Taifa letu.
Kabwe Zuberi Zitto,Mb
Waziri Kivuli Fedha na Uchumi