Zitto na Demokrasia

Zitto na Demokrasia

Posts Tagged ‘Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma

RASIMU YA RATIBA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA MASHIRIKA YA UMMA (POAC)

with 4 comments

LENGO: KUCHAMBUA NA KUJADILI TAARIFA YA HESABU ZILIZOKAGULIWA ZA MASHIRIKA YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA UNAOISHIA JUNI 30, 2010

S/N

TAREHE

SHIRIKA

MHUSIKA

1 Jumamosi na Jumapili 22 -23 Oktoba Wajumbe kuwasili Dar es salaam  

 

 

 

 

 

  • WAJUMBE WA KAMATI
  • OFISI YA CAG
  • WENYEVITI WA BODI ZA MASHIRIKA HUSIKA
  • WATENDAJI WA MASHIRIKA
  • MSAJILI WA HAZINA

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

2 Jumatatu 24 Oktoba
  1. Bodi ya Utalii Tanzania ( TTB)
  2. Benki ya Posta Tanzania ( TPB)
3 Jumanne 25 Oktoba  

  1. kituo cha uwekezaji Tanzania ( TIC)
  2. Mfuko wa Pensheni ya Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa ( LAPF)
4 Jumatano 26 Oktoba
  1. Mamlaka ya Ufundi stadi Tanzania ( VETA)
  2. Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma ( PPF)
5 Alhamisi 27 Oktoba
  1. Shirika la Mafuta Tanzania ( TPDC)
  2. Chuo cha Uhasibu Arusha
  3. Chuo kikuu cha Ardhi
6 Ijumaa 28 Oktoba
  1. Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji ( EWURA)
  2. Shirika la Madini Tanzania ( STAMICO)

 

 

7 Jumamosi na Jumapili 29 – 30 Oktoba Mapumziko ya Mwisho mwa wiki

 

 

8 Jumatatu 31 Oktoba        1.   Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu ( HESLB)

2.  Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania ( TANESCO)

 

9 Jumanne 01 Novemba
  1. Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)
  2. Maktaba kuu ya Taifa

 

10 Jumatano Novemba 02
  1. Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano ( TCRA)
  2. Tume ya Taifa ya Mipango ya Ardhi
  3. Chuo kikuu Dodoma
11 Alhamisi Novemba 03       1.Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB)

2. Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini ( IRDP)

 

12 Ijumaa Novemba 04
  1. Benki ya Twiga ( TWIGA BANCORP)
  2. Bodi ya Pamba Tanzania
  3. Chuo cha Taifa cha usafirishaji ( NIT)

 

13 Jumamosi na Jumapili 05 – 06 Novemba Kuelekea Dodoma Katibu wa Bunge

 

TANBIHI          

  • Saa 3:00 Asubuhi: kuanza Kwa kikao
  • Saa 4:00 Asubuhi: chai

 

Written by zittokabwe

October 25, 2011 at 12:40 PM

Press Release: Mkulo apishe uchunguzi

with 4 comments

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Waziri wa Fedha ndugu Mustafa Mkulo akae pembeni kupisha uchunguzi dhidi yake kuhusu Shirika la CHC.

Katika Mkutano wa Nne wa Bunge la Kumi kulitokea malumbano makali kati ya  Serikali na Wabunge wajumbe wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma kuhusu kuongezwa muda wa Shirika la CHC. Wakati Waziri wa Fedha alileta Azimio la kulivunja Shirika hili lenye taarifa nyingi na nyeti kuhusu zoezi la Ubinafsishaji, Kamati ya Bunge ya POAC kutokana na uzoefu wake wa kukagua mahesabu ya Mashirika ya Umma na kufuatilia zoezi la Ubinafsishaji wa Mashirika ya Umma, ilipinga hatua hii na kulitaka Bunge kukataa Azimio la Serikali na kulifanyia marekebisho makubwa. Hatimaye Bunge liliridhia kufanya mabadiliko makubwa katika Azimio la CHC, kwa kuamuru Shirika lipewe uhai wa miaka 3 na kuagiza uchunguzi wa namna bora ya kuendesha shughuli za Shirika la Consolidated Holdings. Mapendekezo ya Kamati ya POAC ni kulifanya Shirika hili kuwa la kudumu na kulipa jukumu la kumiliki na kusimamia uwekezaji wa Serikali kwenye kampuni binafsi (National Investment Agency) kama ilivyo Shirika la Tamasek ya Singapore na Shirika la Khazana ya Malaysia. Kwa sasa Uwekezaji wa Serikali katika Kampuni binafsi unasimamiwa na Hazina na usimamizi wake ni mbovu na hauleti tija kwa Taifa.

Kitendo cha kushindwa kwa hoja Bungeni kiliifedhesha Serikali na hivyo kwa kupitia Wizara ya Fedha kuamua kulihujumu Shirika kwa kumsimamisha Mkurugenzi wake Mkuu kwa makosa ya kimajungumajungu na kwa kuzusha kwamba CHC iliwahonga wabunge ili kuitetea.  Waziri wa Fedha ndugu Mustafa Mkulo alilitaarifu Bunge kuwa Bodi ya CHC imeomba ukaguzi maalumu kuhusu tuhuma za ubadhirifu ndani ya Shirika hilo. Niliitaka Serikali ichunguze pia tuhuma kwamba Kamati ya POAC ilihongwa na kuahidi kuahidi kujiuzulu nyadhifa zangu zote ikithibitika.

Katika Uchunguzi wake Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Heabu za Serikali kwa kupitia Kampuni ya Ernest and Young walitaka kufanya mahojiano na Waziri wa Fedha juu ya tuhuma mbalimbali zinazomkabili ndani ya CHC. Waziri Mkulo alikataa kuhojiwa na wakaguzi na badala yake akaandika barua (kumb TYC/B/70/2/03 ya Oktoba 8, 2011) yenye kujibu tuhuma moja, tena kwa juu juu, kuhusu yeye kuliamuru Shirika kuuza kiwanja cha Shirika bila kufuata taratibu za sheria. Wakati Waziri anakanusha kuliagiza Shirika kuuza kiwanja kwa mtu aliyemtaka yeye, mimi nina ushahidi tosha wa Nyaraka kutoka Hazina, kwa mfano barua TYC/A/290/13/4 ya Machi 9, 2011 ambayo inawagiza CHC kutekeleza agizo la Waziri la Fedha kuhusu kiwanja na. 10 barabara ya Nyerere. Vilevile, nina ushahidi wa mkutano uliofanyika huko Morogoro Hotel kati ya Waziri wa Fedha na Mwenyekiti wa Bodi ya CHC kuhusu jambo hilo.

Siku mbili baada ya kumjibu CAG, Waziri wa Fedha ndugu Mustafa Mkulo aliamua kutengua uamuzi wake wa kuongeza muda wa Bodi ya Shirika la CHC mpaka mwezi Disemba 2011 na hivyo kuivunja. Uamuzi huu wa Waziri una lengo la kuficha ukweli kwani CHC bila Bodi ya Wakurugenzi inaendeshwa na Hazina na hivyo taarifa ya ukaguzi itabidi ipelekwe Hazina ambayo Waziri wake ni mtuhumiwa.

Uchunguzi wa kina

Ninapendekeza uchunguzi wa kina ufanyike kwa kutumia vyombo vya dola na hasa TAKUKURU kuhusu tuhuma hizi dhidi ya Waziri wa Fedha na alazimishwe  kisheria kujibu maswali ya wakaguzi (Auditors) kuhusu tuhuma dhidi yake.

Wakati uchunguzi unaendelea ndugu Mustafa Mkulo asimamishwe kazi ya Uwaziri wa Fedha hadi hapo uchunguzi utakapokamilika. Kitendo chake cha kuiamuru Bodi kumsimamisha kazi aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu kwa tuhuma za kutunga na majungu na baadaye kuvunja Bodi ya CHC wakati inasubiri taarifa ya uchunguzi kutoka kwa CAG ni kuingilia uchunguzi na pia ni matumizi mabaya ya Ofisi ya Umma ili kulinda maslahi binafsi. Ni dhahiri akiendelea kuwa Waziri wa Fedha ataharibu uchunguzi.

Vilevile, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu Jakaya Kikwete aangalie kama anaitendea haki nchi na Uchumi wa nchi kwa kuwa na Waziri wa Fedha ambaye anasema uwongo Bungeni bila kuogopa na mwenye kutumia Ofisi yake vibaya kwa kuchukua maamuzi yanayoingilia uchunguzi unaomhusu ili kujilinda.

Taarifa ya Uchunguzi ikabidhiwe kwa Spika

Kutokana na ukweli kwamba suala la CHC lilianzia Bungeni na hata Waziri mwenyewe kukiri kuwa taarifa ya uchunguzi inapaswa kuwekwa wazi. Kutokana na matokeo ya sasa ambapo Waziri wa Fedha mwenyewe ana tuhuma za kujibu na kwamba hivi sasa hakuna Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika na hata itakayoundwa itateuliwa na Waziri mtuhumiwa ninashauri kuwa taarifa ya uchunguzi wa Shirika la CHC sasa ipelekwe kwa Spika wa Bunge kwa hatua zaidi.

Kabwe Zuberi Zitto, Mb

Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi

Dar es Salaam, 13 Oktoba, 2011.