Wabunge wapiga sahihi kutokuwa na imani na Pinda #voteofNOconfidence
Deo akitia sahihi
Mbunge wa Ludewa (CCM), Deo Filikunjombe akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma jana. Kulia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe anayefanya zoezi la kukusanya sahihi za wabunge ili aweze kuwasilisha bungeni hoja kutokuwa na imani na waziri mkuu, Jumatatu wiki ijayo.
Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, katika Ofisi ya Kambi ya Upinzani Bungeni mjini Dodoma jana. Kushoto ni Msaidizi katika ofisi ya kami hiyo, John Mrema.
Mbunge wa wa Kasulu Mjini, Moses Machali akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ndani ya ukumbi wa Bungeni mjini Dodoma jana. Kushoto ni Mbunge wa Kigoma Kusini, Zitto Kabwe anayetaka kuwasilisha bungeni hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu.
Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ndani ya ukumbi wa Bungeni mjini Dodoma jana.
Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ndani ya ukumbi wa Bungeni mjini Dodoma jana.
huo ndio utendaji. Asiyewatumikia watanzania kwa moyo wote na kukalia udokozi basi abebe msalaba wake atupishe. Mh. Zitto keep it up man!!
mhuli lyehagi
April 22, 2012 at 7:23 AM
Mh. Zitto Kabwe,
Nakupongeza sana kwa hiyo hatua yako si tu italeta mabadiliko katika nchi bali italeta funzo kwa mawaziri wengine katika utendaji wao wa siku kwa siku! Lakini pia nimefurahi kwani hiyo hatua yako itapambanua wabunge wa CCM wanafiki na wasio wanafiki.
Mimi, naamini na watanzania wengine wanaochukizwa kidhati na mambo ya serikali yetu, tunakuombea kwa Mungu ili katika hili daima msirudi nyuma ila msimame mpaka kieleweke. Naamini Mungu atawasaidia kwani kila anayepigania haki kwa hali yoyote ile hufanikiwa.
Kazi Njema
Gaston Mbilinyi
April 22, 2012 at 10:02 AM
Hakika tungekuwa na watu 10 tu sirious kama wewe bungeni wao mawazir wangenyoka kiukweli kaka tunakuombea kwa mungu sana
I 2the nandumbi
April 22, 2012 at 3:37 PM
hongera sana kamanda wapeleke hao.mafisadi
yue
April 23, 2012 at 12:04 PM
Hili ndio bunge tunalolihitaji lenye kuwa na wabunge wasiokuwa na uwoga na wenyekupambanua mambo kiundani kwa maslahi ya nchi yao huo ndio uzalendo
Luggy boy
April 24, 2012 at 12:37 PM
Hili ndio bunge tunalolihitaji lenye kuwa na wabunge wasiokuwa na uwoga na wenyekupambanua mambo kiundani kwa maslahi ya nchi yao huo ndio uzalendo.Hongera sana Zitto Kabwe wewe ni mwamba tunakutegemea watanzania hakika wewe ni kioo cha watanzania
Luggy boy
April 24, 2012 at 12:50 PM
wenyekupambanua mambo kiundani kwa maslahi ya nchi yao huo ndio uzalendo.Hongera sana Zitto Kabwe wewe ni mwamba tunakutegemea watanzania hakika wewe ni kioo cha watanzania
Luggy boy
April 24, 2012 at 12:53 PM
[…] the process of the collection of signatures for the Vote of NO Confidence The Guardian quoted me on April 22 for crediting the Norwegian government for incitement to take […]
#sahihi70 – where did the inspiration come from? « Zitto na Demokrasia
May 8, 2012 at 1:40 PM