Zitto na Demokrasia

Zitto na Demokrasia

Wabunge wapiga sahihi kutokuwa na imani na Pinda #voteofNOconfidence

with 8 comments

Deo akitia sahihi
Mbunge wa Ludewa (CCM), Deo Filikunjombe akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma jana. Kulia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe anayefanya zoezi la kukusanya sahihi za wabunge ili aweze kuwasilisha bungeni hoja kutokuwa na imani na waziri mkuu, Jumatatu wiki ijayo.

Kangi Logola akiweka sahihi
Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, katika Ofisi ya Kambi ya Upinzani Bungeni mjini Dodoma jana. Kushoto ni Msaidizi katika ofisi ya kami hiyo, John Mrema.
Machali wa NCCR akiweka sahihi
Mbunge wa wa Kasulu Mjini, Moses Machali akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ndani ya ukumbi wa Bungeni mjini Dodoma jana. Kushoto ni Mbunge wa Kigoma Kusini, Zitto Kabwe anayetaka kuwasilisha bungeni hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu.
Mbowe akiweka Sahihi
Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ndani ya ukumbi wa Bungeni mjini Dodoma jana.
Mrema wa TLP akiweka sahihi
Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ndani ya ukumbi wa Bungeni mjini Dodoma jana.
Kahigi wa Chadema akiweka sahihi
Mbunge wa Bukombe, Prof Kulikoyela Kahigi akiweka sahihi katika fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Katikati ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari.

Written by zittokabwe

April 21, 2012 at 9:15 PM

Posted in Uncategorized

Tagged with

8 Responses

Subscribe to comments with RSS.

  1. huo ndio utendaji. Asiyewatumikia watanzania kwa moyo wote na kukalia udokozi basi abebe msalaba wake atupishe. Mh. Zitto keep it up man!!

    mhuli lyehagi

    April 22, 2012 at 7:23 AM

  2. Mh. Zitto Kabwe,

    Nakupongeza sana kwa hiyo hatua yako si tu italeta mabadiliko katika nchi bali italeta funzo kwa mawaziri wengine katika utendaji wao wa siku kwa siku! Lakini pia nimefurahi kwani hiyo hatua yako itapambanua wabunge wa CCM wanafiki na wasio wanafiki.

    Mimi, naamini na watanzania wengine wanaochukizwa kidhati na mambo ya serikali yetu, tunakuombea kwa Mungu ili katika hili daima msirudi nyuma ila msimame mpaka kieleweke. Naamini Mungu atawasaidia kwani kila anayepigania haki kwa hali yoyote ile hufanikiwa.

    Kazi Njema

    Gaston Mbilinyi

    April 22, 2012 at 10:02 AM

  3. Hakika tungekuwa na watu 10 tu sirious kama wewe bungeni wao mawazir wangenyoka kiukweli kaka tunakuombea kwa mungu sana

    I 2the nandumbi

    April 22, 2012 at 3:37 PM

  4. hongera sana kamanda wapeleke hao.mafisadi

    yue

    April 23, 2012 at 12:04 PM

  5. Hili ndio bunge tunalolihitaji lenye kuwa na wabunge wasiokuwa na uwoga na wenyekupambanua mambo kiundani kwa maslahi ya nchi yao huo ndio uzalendo

    Luggy boy

    April 24, 2012 at 12:37 PM

    • Hili ndio bunge tunalolihitaji lenye kuwa na wabunge wasiokuwa na uwoga na wenyekupambanua mambo kiundani kwa maslahi ya nchi yao huo ndio uzalendo.Hongera sana Zitto Kabwe wewe ni mwamba tunakutegemea watanzania hakika wewe ni kioo cha watanzania

      Luggy boy

      April 24, 2012 at 12:50 PM

      • wenyekupambanua mambo kiundani kwa maslahi ya nchi yao huo ndio uzalendo.Hongera sana Zitto Kabwe wewe ni mwamba tunakutegemea watanzania hakika wewe ni kioo cha watanzania

        Luggy boy

        April 24, 2012 at 12:53 PM

  6. […] the process of the collection of signatures for the Vote of NO Confidence The Guardian quoted me on April 22 for crediting the Norwegian government for incitement to take […]


Leave a comment