Zitto na Demokrasia

Zitto na Demokrasia

Posts Tagged ‘Askari wa Polisi

Mhamiaji Haramu? #WahamiajiHaramu cc @hrw @refugees @amensty

with 5 comments

This old man lives in Kigoma with documents from UN as a refugee. The govt denies that it doesn’t deport such people. This is an evidence of a person dumped at DR Congo Embassy in Kigoma. Interestingly during elections CCM gives membership cards to refugees to vote for them as evidenced here.

For how long will Tanzania lives in state of denial?

 

Familia moja kwa wazazi wote 2 haiwezi kuwa na baadhi wahamiaji haramu na baadhi Watanzania. Lakini kutokana na kukamata watu hovyo kunakofanywa na Askari wa Polisi, Uhamiaji na JWTZ huko Kigoma inawezekana.

 

Mzee huyu alikamatwa akitoka porini kuchimba dawa. Amekamatwa na familia yake nzima. Alihukumiwa ni mhamiaji haramu hata kabla ya kuhojiwa. Kosa lake? Mmanyema. Askari wakikumata ukasema wewe ni Mmanyema au Mbembe unaitwa mkongo. Ukisema wewe Muha unaitwa Mrundi. Operesheni ya wahamiaji haramu itaacha mtu Kigoma?

 

Mama huyu kakamatwa kama mhamiaji haramu na kupelekwa Ubalozi mdogo wa DR Congo uliopo Manispaa ya Kigoma. Amezaliwa Tanzania, amesomea Tanzania, Baba yake Mtanzania, Babu yake Mtanzania na Ndugu zake wengine Watanzania na hawakukamatwa. Amekamatwa akitoka kuchota maji ziwani Tanganyika. Malalamiko yake nimeyafikisha kwa Waziri wa Mambo ya Ndani.

Written by zittokabwe

September 16, 2013 at 11:16 AM