Zitto na Demokrasia

Zitto na Demokrasia

Posts Tagged ‘Tabora

AZIMIO LA TABORA 2015 @ACTWazalendo

with 3 comments

Written by zittokabwe

June 15, 2015 at 6:56 AM

Siku ya 7 CHADEMA Kanda ya Magharibi- Jimbo la Bukene, wilaya ya Nzega

leave a comment »

Timu ya CHADEMA kanda ya Magharibi ikijumuisha Mwenyekiti wa Kanda Ndg. Mambo na Wenyeviti wa Mikoa 3 ya Kigoma, Tabora na Katavi tumetembelea Jimbo la Bukene, wilaya ya Nzega.
Kama ilivyo kwa mikutano iliyopita tumezungumza umuhimu wa Katiba na mchakato wake kutopendelea chama chochote cha siasa kwani tunaandika katiba ya nchi, umuhimu wa mwafaka wa kitaifa na kuwapongeza viongozi wakuu wa vyama kwa kukubali kufanya mazungumzo ili kupata mwafaka. Pia tuliwaambia wananchi wasikubali mbinu chafu za kutaka kuongeza muda wa Bunge mpaka 2017 kwani itakuwa ni kinyume na katiba yenyewe.
Wananchi wa Bukene ni wakulima wa Pamba na sehemu kidogo Tumbaku. Kioja tulichokikuta Bukene ni wananchi kuuziwa dawa za Pamba feki ambazo haziui wadudu! Wananchi wa vijijini wanafanyiwa kila aina ya dhulma na kukandamizwa.
Pia tulielezwa namna watendaji wa vijiji na kata wanavyonyanyasa raia kwa kujifanya wao wakamataji, waendesha mashtaka na mahakimu. Wanatoza faini wananchi kwa kesi za kubambika. Itabidi tutafute namna ya kuhakikisha hatua zinachukuliwa dhidi ya watendaji wa kata na vijiji wanaokiuka misingi ya utawala bora. Wananchi wa vijijini wana haki ya kuishi kama raia wengine wa Tanzania. Tusiwasahau

This slideshow requires JavaScript.

Written by zittokabwe

October 12, 2013 at 9:21 AM

Siku ya Nne ya ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi -Wilaya ya Sikonge Mkoa wa Tabora

with 2 comments

Siku ya Nne ya ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi imetupeleka Wilaya ya Sikonge Mkoa wa Tabora.

Nikiwa na Wenyeviti wa chama wa mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora pia Mwenyekiti wa Kanda ya Magharibi Ndg. Mambo tumefanya mikutano 4.

MAJI

Kata ya Kitunda nilivunjika moyo sana baada ya kushuhudia wananchi wakichota maji ya Kunywa kwenye dimbwi ambamo Ng’ombe anakunywa maji. Maji yana rangi kama chai ya maziwa. Nimevunjika moyo sana sababu kwa umri huu wa Taifa letu Maji safi na salama haipaswi kuwa ni jambo la kukampenia tena au kufanyia siasa. Kina mama wanatembea kilometa nyingi kwenda kuchimba maji kwenye madimbwi. Watanzania hawastahili kabisa maisha ya namna hii. Nimepata uchungu sana sababu hizi ndio kazi wanasiasa tunapasa kufanya kusaidia wananchi na kwa kweli kukutana na hali kama hii kunavunja moyo sana.

Baadhi ya Wabunge tulisimama kidete kuhakikisha bajeti ya Wizara ya Maji inaongezwa na ikaongezwa TZS185 bilioni kwa ajili ya Maji vijijini. Ni wajibu wetu wabunge kuhakikisha fedha hii inafika kwa wananchi ili kuwaondolea madhila haya wasiostahili. Changamoto kama hizi za wananchi masikini wa vijijini zinanifanya nifikirie sana nafasi yangu binafsi katika siasa za nchi yetu, siasa za masuala na majawabu.

This slideshow requires JavaScript.

 

Kero ya Wakulima wa Tumbaku

Kero ya wakulima wa Tumbaku bado ni kubwa sana na tumekuwa tunaelezwa kila tunapokwenda. Hapa Sikonge mwaka 2012/13 Chama Kikuu cha Ushirika kimewakata wananchi fedha za mbolea ambayo wananchi hawakupata. Wananchi wanakaa msimu mpaka msimu kupata fedha za mauzo ya Tumbaku. Makato ni mengi na kufanya mkulima ashindwe kuvunja mzunguko wa umasikini.

Nimetoa mawazo ya kisera kwamba imefikia wakati wakulima kupitia vyama vya msingi wajiunge na mifuko ya hifadhi ya jamii ili kuweza kwanza kuweka akiba, pili kupata mikopo nafuu kupitia vyama vyao vya kuweka na kukopa na hivyo kuweza kuwalipa wakulima pindi wauzapo tumbaku.

Nimetoa wito kwa SSRA waangalie uwezekano wa kuanzisha scheme maalumu ya hifadhi ya jamii kwa wakulima ambapo Serikali ishiriki kwa kuchangia kiwango maalumu katika kila michango ya wakulima. Hii itawezesha wakulima kupata mafao kama bima ya afya, bima ya mazao, mikopo midogo midogo, tofauti za bei na hata elimu kwa watoto wategemezi. Hili ni wazo jipya lakini linapaswa kutazamwa ni kuinua wakulima wa Tanzania. Tusiendelee kuwasahau wakulima. Watanzania wapo Vijijini, tusiwasahau. Umasikini wa Tanzania unaonekana vijijini (rural phenomenon), tutokomeze umasikini kwa kuwekeza kwa mkulima.

This slideshow requires JavaScript.

 

 

Written by zittokabwe

October 9, 2013 at 7:10 AM