Archive for the ‘Tanzania’ Category
Magufuli a transformative or a perfectionist of status quo? @TheCitizenTZ @ACTWazalendo @ZittoKabwe
By Zitto Kabwe, MP
General election of 2015 was one of the toughest in Tanzanian history. John Magufuli, a candidate of the ruling party won the election with the lowest proportionate of votes than any other since introduction of multiparty elections in 1995. With 58% of votes, he assumed power and quickly established himself as the landslide victor. President Magufuli started to take actions that sent clear message that his was not a business as usual administration.
For the people who have been advocating for a clean government by fighting corruption especially large scale ones, Magufuli was a welcome leader. Many of us celebrated his actions popularly known as ‘ kutumbua majipu’ and as of the date of writing this article more than 150 people have been sacked from their positions of power. Most notable sackings were at port authority and revenues authority. Achivements received in his first month was massive increase of government monthly revenues collections.
The President delivered his maiden speech in parliament that insisted largely on his anti corruption platform and his aim of cutting down unnecessary government expenditures, boosting revenues and industrialization of the economy. He became a talk of the region and sometimes globally. The Economist magazine dedicated an article for him vis a vis a rise of social media in politics ( though everybody knows that he himself is not a tech savy person ).
Has 100 days of Magufuli administration defined him of what kind of a leader he is? Can we call him a transformative leader? Is he a reformer? Is he just a perfectionist of the status quo?
Archie Brown in his seminal book The Myth of the Strong Leader, describe a transformational leader as ‘the one who plays a decisive role in introducing a systemic change’ whether of the political or economic system of his or her country. ‘ It suggests profound change, but a fundamental reconstruction of the system into one that is qualitatively better than what has gone before’. It may be very early (just 100 days) to define President Magufuli, however the first 100 days may help us to see what kind of a President Magufuli will become.
Magufuli took office with a promise of Change. His opponents promised change too. The political group that was a leading opponent had a clear message that it wanted to change the system and they often referred to ‘corrupt system’ or corruption is systematic. Has President Magufuli’s actions against corruption bear any semblance of breaking down a corrupt system? He has fired people and try some in the court of law. He even fired an anti corruption czar Dr. Edward Hosea. We have seen people removed and others replaced and installed. Has PCCB and other accountability agencies changed? These are key questions, very fundamental in analyzing President Magufuli.
Our system is characterized by impunity. President Magufuli’s actions have shown that everybody must live in accordance to the law. However he hasn’t done anything to reform the agencies that uphold rule of law and law enforcement. PCCB is still the same. It has no powers to prosecute without permission from the Director of Public Prosecution ( DPP ). In his first 100 days not only has President Magufuli been quite of reforming the institutions, we have seen two parliamentary sessions without any legislation to that effect. Changing heads of these institutions means the President is interested with perfecting the existing system rather than transforming the system that brought him to power.
#WhatWouldMagufuliDo became a trending hashtag in twitter. There exists in people’s spirits someone named Magufuli and like a personality cult is being developed. All his ministers are asking themselves ‘ is this the way in which the people expect Magufuli to act? In this regard we have observed a growth of one man show and two principle leaders of the country The Vice President and the Prime Minsiiter being eclipsed. A personality whose work is supposed to be ‘office work’ in the name of Chief Secretary of the country has turned a celebrity. He is being seen making announcements to sack that and change that and early in this administration the Chief Secretary was seen inspecting hospital beds in Muhimbili. Chief Secretary as the disciplinary authority of the bureaucrats shall never be the prosecutor since the people he announces sacking would end up in his desk for appeals. Slowly the country is heading towards a One Man Show and all others ‘Presidents Men’. It is a worrying trend being observed in his first 100 days and it must be stopped.
The third phase administration under President Mkapa didn’t allow dissent opinion. Records show that for five years President Mkapa and Prime Minister Sumaye didn’t allow reports of the Controller and Auditor General to be debated in Parliament an important step in building accountability in the country. Works of Public Accounts Committees of Parliament were suppressed and Parliament became largely a rubber stamp of the works of the executive. President Kikwete changed that and strengthened the Office fo the National Audit, allowed Parliament to debate CAG reports and even took actions against Ministers whose ministries had poor financial records. Signs are that President Magufuli will not allow this continue. The formations of committees done recently point to that direction. As far as parliamentary accountability is concerned, this will be a backward move against all the achievements recorded thus far.
My judgment of President Magufuli’s first 100 days is that the status quo will continue with some perfections. More revenues will be collected, service delivery in some sectors of the economy ( health and education ) may improve, old corruption will be addressed with vehemence and new ones emerges with treatment of kids gloves but accountability institutions will be hugely undermined. As for Transformational leader, Magufuli is yet to fit the bill.
——-
Zitto Kabwe@zittokabwe is the Party Leader and MP for Kigoma Urban (ACT-Wazalendo)
Baadhi ya kazi za Zitto Bungeni
Baadhi ya kazi za Zitto Bungeni
Kwa uzito na mahala unapofanyika mkutano huu, naomba niwaletee kwa muhtasari kabisa baadhi ya kazi ambazo Ndugu Zitto Kabwe amezifanya katika kusukuma mbele guruduma la maendeleo katika nchi yetu.
- MABADILIKO SEKTA YA MADINI
Zitto alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuwa mbunge mwaka 2005 akiwakilisha Jimbo la Kigoma Kaskazini ambalo halina mgodi hata mmoja wa madini ukiachana na wachimbaji wadogo wa udongo wa Pemba ambao una soko kubwa hapa Kariakoo jijini Dar es Salaam. Hata hivyo ajenda inayomtambulisha Zitto Kabwe kwa Taifa ni ajenda ya mabadiliko makubwa aliyoanzisha katika sekta ya Madini nyakati ambayo hakuna mwanasiasa aliyethubutu kukosoa sera za uwekezaji kwa namna aliyofanya. Baada ya kudokezwa kuwa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Bwana Nazir Karamagi amesaini mkataba mpya wa Madini akiwa hotelini nchini Uingereza, Zitto alimtaka Waziri kujieleza ndani ya Bunge kuhusu mkataba huo na masharti yake ya kikodi. Waziri huyo aliposhindwa Zitto aliwasilisha Hoja Binafsi Bungeni (akiwa mbunge wa kwanza kufanya hivyo katika Bunge la Tisa na la Nane kwa pamoja). Hoja ya Buzwagi ilisababisha Zitto kusimamishwa ubunge kwa miezi 4. Hata hivyo mnamo Septemba 10, 2007 alitangaza Azimio la Songea lililomshinikiza Rais Jakaya Kikwete kuunda Kamati ya Bomani ili kupitia mikataba yote ya Madini nchini.
Kutokana na kazi yake hiyo leo Tanzania ina Sera mpya ya Madini na Sheria mpya ya Madini ambayo imeboresha nafasi ya Tanzania kufaidika na Madini, imeruhusu kisheria Serikali kuwa na hisa kwenye migodi ( na hivi tunavyoongea, kwa mfano, sasa Serikali inamiliki 50% ya Mgodi wa TanzaniteOne). Makampuni ya Madini ambayo yalikuwa yanatangaza hasara kila mwaka leo yanalipa kodi ya Mapato na Halmashauri zenye migodi zinalipwa ushuru wa huduma wa mabilioni ya fedha. Huyu ndiyo Kiongozi wetu wa ACT Wazalendo. Hawa ndio Viongozi Taifa hili linawataka. Viongozi wanaotenda na kutoa majawabu ya changamoto za nchi. Sio Viongozi wanaolaumu tu eti wakisubiri kushika dola ndio watende. Nani anayebisha rekodi hii?
- KUZUIA UBINAFSISHAJI WA SHIRIKA LA BIMA LA TAIFA (NIC)
Zitto Kabwe alikuwa Waziri Kivuli wa Mipango na Uchumi mwaka 2006 wakati Shirika la Bima la Taifa likiwa kwenye mchakato wa Ubinafsishaji. Wafanyakazi wa TUICO Tawi la Bima walimfuata wakielezea kwa ushahidi namna mali za Shirika zilivyopangwa kuuzwa na wajanja wachache kutaka kujiuzia Shirika na Mali zake hasa jengo la kitega uchumi kwa bei ya kutupwa. Zitto aliwakilisha hoja hiyo kwenye Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi chini ya Mwenyekiti wake Ndugu Abdallah Kigoda na kuishawishi Kamati kukataa ubinafsishaji wa NIC na badala yake kuunda kikosi kazi cha kurekebisha Shirika na liendelee kuwa Mali ya Umma.
Mwezi Novemba Mwaka 2006 Baraza la Mawaziri lilikubaliana na hoja za Zitto alizotoa kwenye Kamati ya Bunge na ndani ya Bunge na kuamua kuliondoa Shirika kwenye mchakato wa ubinafsishaji na leo hii Shirika limebaki kuwa la Umma na limeanza kurudi kwenye hali yake. Aliendelea kulisaidia Shirika la Bima kwa kuagiza (akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali ) kuwa Taasisi za Serikali na Mashirika ya Umma yaweke Bima kupitia Shirika la Bima la Taifa na agizo hilo kutekelezwa na Mashirika mengi ikiwemo Benki Kuu ya Tanzania.
Sio Bima tu, Zitto akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma aliagiza kuondolewa katika orodha ya ubinafsishaji Shirika la STAMICO ili liweze kushiriki kikamilifu katika sekta ya Madini na liliondolewa. Huo ndio Ujamaa wa kidemokrasia ambao Chama chetu cha ACT-Wazalendo kinautangaza, na huyo ndio Kiongozi wetu ambaye ana uzalendo wa dhati kwa mali za Watanzania. Nani anayebisha rekodi hii?
- SHERIA YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA
Mwaka 2008/2009 Zitto Kabwe aliweka rekodi nyingine ya kuwa Mbunge wa kwanza kuzungumzia mabadiliko ya sheria ya viongozi wa umma ili kuipa meno secretariat ya maadili ya viongozi na kutengenisha biashara na siasa. Alipeleka Bungeni Muswada Binafsi wa Sheria ili kufanya mabadiliko makubwa ya Sheria Maadili. Hata hivyo muswada ule ulizuiwa na Serikali kuingia Bungeni licha ya kukamilisha kila hatua iliyopaswa.
Leo hii Chama chetu kinazungumzia kurejesha Miiko ya Viongozi kuna watu wanadhani Zitto kaanza haya hivi sasa, la hasha. Huu ni mwendelezo wa yale aliyokuwa anaamini miaka kadhaa iliyopita na kwa kuwa yeye anapenda kutembea anayoyasema alitushawishi wenzake kufanya Miiko ya Viongozi kuwa sehemu ya Katiba ya Chama chetu. Yeye ni Kiongozi wa kwanza wa kisiasa kuweka hadharani Mali na Madeni yake hapa nchini. ACT Wazalendo ni chama pekee cha siasa hapa nchini ambacho Viongozi wake wanatakiwa kikatiba kutangaza Mali zao, Madeni yao na Maslahi yao ya kibishara. Nani anabisha rekodi hii?
- UKAGUZI WA MAHESABU WA VYAMA VYA SIASA
Katika kuhakikisha kuwa kila senti ya fedha ya umma inakaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali, Ndugu Zitto Kabwe aliwasilisha Bungeni mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa, Sheria namba 5 ya Mwaka 1992 na kuwezesha CAG kukagua fedha za vyama ambazo zinatoka Serikalini kama ruzuku. Sheria ya Vyama vya siasa inataka kila Mwaka Serikali kutenga kiwango kisichozidi asilimia mbili (2%) ya Bajeti ya Serikali kama ruzuku kwa vyama vya siasa. Vyama hupewa wastani wa Shilingi bilioni 20 kila mwaka na kugawana miongoni mwao lakini fedha hizi zilikuwa hazikaguliwi kinyume na Sheria za Fedha.
Baada ya Sheria hiyo kupitishwa na Bunge mwaka 2009, Zitto alisimama kidete kuhakikisha inatekelezwa jambo ambalo lilimletea uhasama mkubwa sana na viongozi wenzake katika chama chake cha zamani akiwa Naibu Katibu Mkuu. Zitto alipigana kwa kushirikiana na Wazalendo wenzake katika Kamati ya Bunge ya PAC na kufanikiwa na hivi sasa vyama vyote vinakaguliwa na kuweka rekodi nyingine katika nchi nyingi za Afrika. Kwa kazi hii iliyotukuka Zitto Kabwe amedhibiti fedha za umma kwa vyama vya siasa na hivi sasa taarifa za mahesabu ya vyama ipo wazi, na tumeona vyama vyote vikiwa na hati chafu, vikiwemo vyama vya upinzani vya zamani. Ni wajibu wa wanachama wa vyama hivyo kuwawajibisha viongozi wao wanaogeuza fedha za ruzuku kuwa ni fedha zao binafsi. Nani anabishia rekodi hiyo ya Kiongozi wetu?
- KUFUFUA ZAO LA MKONGE
Mwaka 2012 Zitto Kabwe aliweka rekodi nyingine tena akiwa mbunge wa kwanza katika Bunge la 10 kuwasilisha Hoja Binafsi. Aliwasilisha Hoja Binafsini Bungeni akitaka Serikali kufufua Kilimo cha Mkonge kwa kuwanyanganya wawekezaji wakubwa mashamba waliyobinafsishiwa na kuyaacha bila kulimwa na badala yake mashamba yale wapewe wakulima wadogo. Zitto alitaka kubadilisha mfumo wa kulima Mkonge kutoka mashamba makubwa yanayomilikiwa na tajiri mmoja na kulimwa na manamba mamia na kwenda kwenye mfumo ambao wakulima wadogo wadogo wanalima Mkonge na hivyo kushirikisha wananchi wengi zaidi kwenye uchumi wao.
Hoja hiyo ilipingwa na Wabunge kutoka Tanga lakini iliungwa mkono sana na wananchi wa mkoa huo na hivyo kumwona Zitto kama mwakilishi wao licha ya kwamba alikuwa akiwakilisha Jimbo la Kigoma Kaskazini.
Katika Chama chetu ajenda ya kumilikisha Ardhi wananchi ni ajenda kubwa na ACT Wazalendo kimekua chama cha kwanza nchini kutangaza kinagaubaga kuwa kitazuia uporaji wa Ardhi na kumilikisha wananchi ardhi yao wenyewe. Nani anabishia rekodi hiyo?
- KURASMISHA KAZI ZA SANAA NA BURUDANI NCHINI
Kwa muda mrefu sana wadau wa tasnia ya sanaa na burudani nchini walikuwa wanalalamika kazi zao kutokuwa rasmi na hivyo kuibiwa na mchango wao katika uchumi kutotambuliwa. Mwaka 2012 Zitto Kabwe akiwa Waziri Kivuli wa Fedha alifanya kampeni maalumu ya kuhakikisha kuwa wasanii hawanyonywi na kazi zao kutambuliwa rasmi. Aliwasilisha Bungeni mabadiliko ya Sheria ya Ushuru bidhaa ili kutambua rasmi kazi za sanaa na burudani na kuhakikisha kuwa wasanii wanalipwa wanavyostahili katika biashara ya miito ya simu.
Sheria hiyo ilipitishwa na Bunge na Mamlaka ya Mapato Tanzania ikaanza kutoa stempu rasmi katika CDs za kazi za sanaa ili kudhibiti wazalishaji kuwanyonya wasanii. Katika Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa ya mwaka 2015 tasnia ya Sanaa na Burudani imekuwa sekta rasmi ya Uchumi na imeripotiwa kuwa sasa ina thamani ya shilingi 270 bilioni kama mchango wake katika Pato la Taifa. Hivi sasa Wasanii wanafaidika maradufu kwa kazi zao kuuzwa kama miito ya simu na wengine wanapata mamilioni ya shilingi na kuboresha maisha yao kwa jasho lao. Nani anabisha rekodi hii?
- KUDHIBITI UKWEPAJI KODI NA MISAMAHA YA KODI
Wawekezaji kutoka nje wamekuwa wakiibia nchi yetu kwa kubadilisha badilisha majina ya makampuni yao na kubadili wamiliki bila ya kulipa kodi hapa nchini. Watanzania mnakumbuka jinsi majina ya mahoteli makubwa yalivyokuwa yakibadilishwa. Kwa mfano kutoka Sheraton kwenda Moevenpick na kwenda Serena sasa. Makampuni ya Simu yalivyokuwa yakibadilishwa. Kwa mfano kutoka Mobitel kwenda Buzz kwenda Tigo.
Vile vile kutoka Celtel kwenda Zain na kwenda Airtel. Haya yamekuwa yakitokea kwenye maeneo mengi zaidi ya haya. Yote haya yalitokea bila ya Serikali kupata kodi yeyote. Kwenye mauzo ya Zain kwenda Airtel Serikali ilipoteza dola za Kimarekani 312 milioni ( zaidi ya shilingi bilioni 600 kwa bei za sasa za dola ). Kwa uchungu kwa nchi yake Zitto Kabwe aliwasilisha Bungeni muswada wa sheria wa kurekebisha sheria ya kodi ya Mapato na kuanzisha tena kodi ya ongezeko la mtaji ( Capital Gains Tax ).
Marekebisho hayo yalipitishwa na Bunge kupitia Sheria ya Fedha ya mwaka 2012 na mwaka huo huo Tanzania ilipata mapato ya shilingi bilioni 50 kwa mauzo ya Kampuni ya BP kwenda PUMA. Mwaka 2014 Tanzania ilipata dola za kimarekani 222 milioni ( zaidi ya tshs 450 bilioni )kwa mauzo ya sehemu ya vitalu vya gesi asilia vya kampuni ya Ophir kwenda kampuni ya Pavilion ya Singapore.
Zaidi ya hapo Zitto na wazalendo wenzake katika Kamati ya PAC walitoa maagizo ya kuhakikisha kuwa Misamaha ya kodi yote inakaguliwa na ukaguzi wake kuwekwa wazi ili kudhibiti mianya ya matumizi mabaya ya misamaha hiyo. Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania CAG anakagua misahamaha ya kodi na PAC iliweka wazi taarifa ya kwanza ya ukaguzi wa misamaha ya kodi. Nani anabishia rekodi hizi?
- MABILIONI YA USWISS
Mwaka 2012 mwezi Novemba Zitto Kabwe aliwasilisha Bungeni Hoja Binafsi kuhusu mabilioni ya Uswisi ikiwa na lengo la kutaka uchunguzi ufanyike kuhusu Watanzania wanaoficha fedha nje ya nchi kinyume cha sheria. Bunge lilipitisha hoja hii binafsi na kuitaka Serikali kufanya uchunguzi kuhusu Watanzania wanaotorosha fedha kwenda nje na kuchukua hatua stahiki za kisheria. Tanzania iliingia katika rekodi ya kuwa nchi ya kwanza katika nchi za Jumuiya ya SADC kupitisha Azimio la Bunge kuhusu suala la utoroshaji wa fedha. Licha ya kwamba Serikali haijatoa taarifa yake miaka miwili sasa toka Azimio la Bunge namba 9 la mwaka 2012, na baada ya danadana ya muda mrefu kutoka vyombo vinavyohusika Kiongozi wetu Zitto Kabwe ameamua leo kupasua jipu la hoja hiyo kwa kuweka wazi orodha ya kwanza ya Watanzania 99 wenye akaunti katika Benki ya HSBC ya Uswiss. Uongozi ni umakini, na sio kukurupuka na kujitafutia sifa za harakaharaka. Ilikuwa ni muhimu Ndugu Kabwe kufuata taratibu zote kabla ya kuanika majina hayo hadharani. Sasa leo baada ya kujiridhisha pasipo shaka atayaanika majina hayo hadharani na wale waliokuwa wanambeza kwamba kashindwa wanyamaze milele! Huyo ndio Zitto, mwenye uvumilivu na ujasiri usio kifani. Anatenda anayosema. Nani anabisha rekodi hii?
- KUWAJIBISHA MAWAZIRI
Katika historia ya Tanzania ni Wabunge wawili tu walioweza kutoa hoja zilizopelekea Mawaziri wengi kuondolewa madarakani kwa mpigo. Ni Zitto Kabwe na Dkt. Harrison Mwakyembe ambaye aliongoza kamati teule ya Bunge iliyochunguza Mkataba wa kampuni feki ya kufua umeme ya Richmond. Hoja hii ilipelekea Waziri Mkuu kuwajibika kwa kujiuzulu na hivyo kumlazimisha Rais wa Jamhuri ya Muungano kuunda upya Serikali kwa kuteua Waziri Mkuu mwingine.
Zitto ana rekodi ya kipekee. Kwanza mwaka 2012 baada ya Taarifa ya CAG kuonyesha madudu katika matumizi ya fedha za umma, Zitto alikusanya sahihi za wabunge 75 na kuandika hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu. Shinikizo hili lilipelekea Rais kufukuza kazi mawaziri 8 ambao Wizara zao zilitajwa kuwa na mahesabu machafu. Pili mwaka 2013 baada ya Kamati ya Mali Asili na Mazingira kutoa taarifa yake Bungeni kuhusu Operesheni Tokomeza, Zitto alisimama ndani ya Bunge na kubadilisha mjadala kwa kutaka Mawaziri wote ambao watendaji wao walitesa wananchi kuwajibika. Mawaziri 4 waliwajibika.
Tatu, mwaka 2014 katika Taarifa Maalumu ya Kamati ya PAC kuhusu uchotwaji wa fedha katika akaunti ya Escrow ya Benki ya Tanzania, Zitto na wazalendo wenzake wa kamati hiyo walipelekea Mawaziri wawili maarufu kama mawaziri wa Escrow na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwajibika. Uwajibikaji umekuwa ni ajenda kubwa ya Kiongozi wetu na amekuwa hana aibu hata kwa watu anaowaheshimu na rafiki zake. Alitaka wawajibike huku akiwatazama usoni. Ni Viongozi wachache sana wenye ujasiri wa aina hii. Huyu ndio Kiongozi wa chama chetu cha ACT Wazalendo. Nani anabisha rekodi hii?
- KUKATAA POSHO ZA KUKAA
Mwaka 2010 chama chake cha zamani waliweka katika Ilani yao ya Uchaguzi kupinga posho kama hatua ya kubana matumizi ya Serikali. Wakakubaliana kuwa wabunge wa chama chao hawatapokea posho ya kukaa (sitting allowance). Hata hivyo, ilipokuja katika utekelezaji wenzake wote wakagwaya na Ndugu Zitto Kabwe ni mbunge pekee aliyepinga posho za vikao na kuzikataa kata kata kwa miaka mitano (5) mfululizo, ambazo ni takribani shilingi milioni 21 kila mwaka. Katika kipindi hicho cha miaka mitano Zitto alikaa kuchukua jumla ya Shilingi Milioni Mia Moja na Tano (105,000,000)!! Kukataa pesa yote hii kwa sababu ya ‘principle’ tu ni jambo nadra sana kutokea katika mazingira yetu. Zitto anatembea maneno yake. Zitto anatenda anayonena. Sasa kwa yote hata kwa nini wasimchukie wenye roho zao za kwa nini?
Ndugu Wananchi,
Huyu ndio Kiongozi wa Chama chetu. Tunachoomba Watanzania mumhukumu Zitto kwa rekodi zake na si kwa propaganda za mahasimu wake.
Tuboreshe Rasimu iliyopo-Zitto Kabwe
Tuboreshe Rasimu iliyopo
Na Zitto Kabwe, MB
Wiki ya Machi 18 – 22, 2014 ilianza kwa siku ya Jumanne Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Sinde Warioba aliwaslisha rasmi Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Bunge Maalumu la Katiba. Wiki hiyo imeishia kwa siku ya Ijumaa Rais wa Jamhuri ya Muungano ndugu Jakaya Mrisho Kikwete kutoa hotuba kwa Bunge Maalumu. Hotuba zote zimepokelewa kwa hisia tofauti kulingana na msimamo wa kila mtu kuhusu hoja inayoonekana ni kubwa
kuliko zote katika mchakato wa kuandika Katiba Mpya – Muundo wa Muungano. Wale wanashabikia muundo wa Serikali Tatu, walifurahishwa mno na hotuba ya Jaji Warioba. Wale wanaoshabikia muundo wa Serikali mbili walifurahishwa mno na hotuba ya Rais Kikwete. Sikufurahishwa na hotuba zote mbili.
Nitaeleza.
Moja, hotuba zote mbili zilichukua muda mrefu zaidi kuelezea sura moja tu ya Rasimu ya Katiba nayo ni sura ya Sita inayohusu muundo wa Jamhuri ya Muungano kana kwamba Katiba hii inahusu suala hilo tu. Ni dhahiri suala hili ni kubwa na muhimu kwani linahusu uhai wa Dola yenyewe na siwezi kubeza. Hata hivyo masuala kama Haki za Raia ni muhimu zaidi kwani hata uwe na muundo wa namna gani wa muungano au hata muungano wenyewe kuvunjika, bila ya kuwa na haki za msingi za raia kwenye katiba katiba hizo zitakataliwa tu na wananchi. Huu mtindo unaozuka wa kudhani muundo wa muungano ndio mwarobaini wa matatizo ya ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka, ubadhirifu, umasikini, elimu ya hovyo, afya dhaifu, utatufikisha pabaya na hata kurudi tena kuandika katiba kudai haki hizo. Jaji Warioba na Rais Kikwete wameshindwa kuruka kiunzi cha kwamba Katiba ni zaidi ya Muungano.
Pili, wote wawili Rais Kikwete na Jaji Warioba wamejenga hoja zao kuhusu miundo ya Muungano wanayopendekeza au kuunga mkono kutokana na misingi ama ya ‘malalamiko’ au ‘hofu’. Jaji Warioba aliorodhesha malalamiko 11 ya upande wa Zanzibar dhidi ya Muungano na malalamiko 10 ya upande wa bara. Kimsingi malalamiko yote ya upande wa bara yanazaliwa na vitendo vya upande wa Zanzibar isipokuwa lalamiko namba vii linalohusu kupotea kwa utambulisho wa Tanganyika katika muundo wa Muungano.
Jaji Warioba anajenga msingi wa pendekezo la Tume yake kutokana na kujibu malalamiko au maarufu kero za Muungano na anasema
“….muundo wa Serikali mbili hauwezi kubaki kwa hali ya sasa. Muungano wa Serikali mbili waliotuchia waasisi siyo uliopo sasa…… waasisi walituachia Muungano wa Nchi Moja yenye Serikali mbili, na siyo Nchi Mbili zenye Serikali Mbili“. Nukuu hii niliipenda kuliko zote katika Hotuba ya Mzee wangu Warioba.
Rais Kikwete alijenga msingi wa maoni yake kwenye hofu za kuwa na Serikali tatu. Hofu hizo ni pamoja na gharama za kuendesha Muungano, kuzuka kwa hisia za Utaifa wa Utanganyika na Uzanzibari, uwezekano wa Muungano kuvunjika kwa kushindwa kuhudumia majeshi na hata Jeshi kuchukua Nchi ikipidi na kutupilia mbali katiba na Serikali ya Muungano kutokuwa na Rasilimali zake. Rais alisema ‘Serikali ya Muungano ni egemezi na tegemezi’ nukuu ambayo niliipenda kuliko zote katika Hotuba ya Mzee wangu Jakaya Kikwete.
Rais Kikwete hakuniridhisha kabisa namna ya kumaliza kero za Muungano kwa muundo uliopo sasa kwani muundo huo umeshindwa kuzimaliza kwa takribani miaka 50 tangu Muungano uundwe. Haiwezekani muundo uliozalisha kero lukuki ndio utarajiwe kuzimaliza kero hizo. Kwa vyovyote vile ni lazima kuwa na muundo mpya lakini kiukweli ni lazima muundo huo mpya ujibu hofu alizoeleza ndugu Rais maana ni hofu za kweli.
Jaji Warioba hakuniridhisha na namna suala la Uraia litakavyotatuliwa kwani kutoa jibu la kubakia na ‘kukubali’ Nchi mbili halafu uraia mmoja kunaleta mashaka makubwa. Kama tunataka kuwa na Uraia mmoja ni lazima tuwe Nchi moja, hatuwezi kuwa na Nchi mbili uraia mmoja.
Vilevile vyanzo vya mapato ya Muungano ni vidogo mno kuendesha dola. Hivyo basi rasimu iliyopo mbele ya Bunge Maalumu ina mapungufu makubwa japo imetoa mapendekezo yatakayomaliza malalamiko ya Muungano.
Sasa kazi ya Bunge ni moja tu nayo ni kuboresha rasimu iliyopo mbeleyake ili kumaliza kero za muungano zilizopo na kujibu hoja za hofu za muundo mpya. Hakuna sababu ya kubishana kwenye takwimu za Tume, tume imefanya wajibu wake na sasa Bunge Maalumu nalo litimize wajibu wake.
Iwapo kama kweli tunataka kusikia Watanzania wanataka nini kwenye muundo wa Muungano, tusimamishe Bunge na twende tukawaulize kwa kura (referendum). Vingivenyo tuboreshe rasimu iliyopo na iliyotokana na maoni ya wananchi wote kwa kujibu hizo hofu muhimu alizoainisha ndugu Rais na hayo malalamiko muhimu yaliyoainishwa na Tume. Sio kazi ya Bunge Maalumu kutafuta ubora wa hotuba zilizotolewa mbele yetu bali kuona mazuri ndani ya hotuba hizo yasaidie kazi yetu Tuzingatie kuwa tusijenge Nchi kwa kujibu malalamiko na hofu tu maana hofu na malalamiko hayaishi katika dunia inayobadilika kwa kasi sana.
Tuamue tunataka kuwa Jamhuri ya Muungano ya namna gani. Nini sababu ya Jamhuri yetu na aina gani ya Tanzania tunataka kujenga. Tuanze kwa kutafsiri sababu ya Tanzania kuwepo na Tanzania gani tunataka kujenga kisha tutunge Katiba itakayowezesha kutufikisha huko tutakapo kufika.
Malaysia na Tanzania: kuelekea Maisha bora dhidi ya kuelekea Ufukarishwaji kupitia Kilimo
Zitto Kabwe, Mb
Wakati Jamhuri ya Tanganyika inapata Uhuru mwaka 1961, Nchi ya Malaya ilikuwa tayari ina uhuru miaka mine kabla. 1957. Malaya ilijiunga na Singapore, Sabah na Sarawak tarehe 16 Septemba mwaka 1963 kuunda Malaysia. Tanganyika ilijiunga na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka miezi saba baadaye. Hata hivyo Singapore ilifukuzwa kutoka katika Muungano wa Malaysia mwezi Agosti mwaka 1965 kutokana na kutofautiana kwa sera kuhusu watu wa asili na namna ya kuwalinda kiuchumi. Viongozi wa Kuala Lumper walitaka kuweka sera za kusaidia wazawa kwa kuwapa upendeleo maalumu wakati viongozi wa Singapore chini ya Lee Kuan Yew walitaka kuwepo na Malaysia moja kwa wote bila upendeleo maalumu kwa Bumiputera (son of the soil). Singapore ina wakazi wengi zaidi wahamiaji kutoka China. Tanzania imeendelea kudumu na Muungano licha ya changamoto kadha wa kadha zinazoukabili muungano huo. Tanzania na Malaysia zote zilitaliwa na mkoloni Mwingereza.
Wakati Tanzania inapata inaundwa mwaka 1964 pato la wastani la mtu mmoja lilikuwa dola za Marekani 63 wakati Malaysia ilikuwa na pato la dola za Marekani 113 Kimsingi nchi hizi zilikuwa sawa kimaendeleo ingawa Tanzania ni kubwa kwa zaidi ya mara tatu ya Malaysia. Hivi sasa Malaysia kipato cha wastani cha mwananchi ni dola za Marekani 10,000 na Tanzania ni dola za Marekani 600. Kwa Tanzania pato la wastani limeongezeka mara kumi takribani na kwa Malaysia limeongezeka mara elfu moja. Nini tofauti ya mikakati ya maendeleo ya nchi hizi mbili?
Leo tutaangalia eneo moja tu la Kilimo na namna Kilimo kilivyoweza kuivusha nchi ya Malaysia na Kilimo hicho hicho bado hakijaweza kuivusha Tanzania. Malaysia iliunda Shirika la Umma linaloitwa Federal Land Development Authority (FELDA) likiwa na wajibu mmoja mkubwa wa kuhakikisha wananchi masikini wanapata ardhi, wanalima kisasa na kuongeza uzlishaji kasha kufuta umasikini. Kila mwananchi masikini aligawiwa ardhi hekta 4.1, ardhi ikasafishwa na kuwekwa miundombinu yote muhimu, ikapandwa michikichi na Mwananchi akapata huduma za ugani ili kukuza michikichi hiyo. Shughuli zote hizi zilifanywa kwa gharama za Serikali na wananchi wale wakapewa kama mkopo ambao walikuwa wanaulipa kidogo kidogo kila wanapovuna na kuuza ngazi/mawese kwa Shirika hili la Serikali. Hivi sasa Shirika hili ni kubwa sana, lina thamani ya dola za kimarekani bilioni 3.5 na kupitia Ushirika wao wananchi hawa waliopewa ardhi ya kulipa michikichi sasa wanamiliki asilimia 20 ya Shirika hili. Malaysia iliweza kuondoa umasikini kutoka asilimia 57 ya wananchi wanaoishi kwenye dimbwi la umasikini mwaka 1965 mpaka chini ya asilimia 3 mwaka 2012. FELDA sasa ni Shirika la kimataifa maana linaanza kuwekeza duniani kote. FELDA ilipouza hisa zake kwenye masoko ya mitaji, IPO yake ilikuwa ni ya tatu kwa ukubwa baada ya Facebook na Japanese Airlines. Shirika la Umma linalomilikiwa na Serikali, Wakulima na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (EPF) na linaloendeshwa kwa misingi ya utawala bora wa makampuni limeweza kufuta umasikini kwa zao moja tu la Michikichi. Malaysia leo inaongoza kwa kuuza Mawese duniani. Michikichi hiyo ilitoka Kigoma, Tanzania na kupelekwa Malaya na Waingereza miaka ya hamsini.
Tanzania nasi tulikuwa na Shirika la Umma kwa ajili ya Kilimo. Leo tuchukulie Shirika la NARCO. Kama FELDA, NARCO walichukua ardhi kubwa maeneo kadhaa nchini. Tofauti na FELDA wao walilima wenyewe mashamba haya na kuweka miundombinu ya kilimo. Tuchukulie mfano wa Mashamba ya mpunga kule Kapunga, wilaya ya Mbarali mkoa wa Mbeya. Mwaka 1985 NARCO walikwenda kijijini Kapunga kuwaomba wananchi wawape ardhi ya kulima mpunga. Wananchi wakawapa hekta 3000 hivi kwa mujibu wa muhtasari wa mkutano mkuu wa Kijiji nilionyeshwa mwaka 2009 nilipoenda kutembelea mashamba haya kufuatia mgogoro wa ubinafsishaji. NARCO wakapata msaada kutoka Serikali ya Japani na uwekezaji mkubwa ukafanyika ikiwemo kuweka kinu cha kukoboa mpunga cha kisasa kabisa. Hata hivyo NARCO ilijiendesha kwa hasara na ilipofika kati kati ya miaka ya 90 ikaamuriwa kubinafsishwa. NARCO ikauza mashamba yale kupitia Mpango wa ubinafsishaji kwa kampuni binafsi. Katika uuzaji huo NARCO waliuza hekta 3500 badala ya 3000 walizopewa na wananchi. Kwa maana hiyo Kijiji cha Kapunga nacho kiliuzwa!
Mifano hii miwili inaonyesha tofauti kubwa za kifikra kimaendeleo kati ya nchi zetu hizi mbili. Moja iliwezesha wananchi kumiliki ardhi na imefanikiwa. Nyingine iliamua kufanya kupitia Shirika la Umma na baada ya kushindwa, badala ya kurejesha ardhi kwa wananchi na kuwawezesha kulima, ardhi ile ikauzwa kwa kampuni ya mtu mmoja. Mfano wa Kapunga upo pia huko Wilayani Hanang kwenye mashamba ya Ngano ya Basotu nk. Hata kwenye mpango wa SACGOTT bado fikra ni za wakulima wakubwa wenye mashamba makubwa badala ya kuwezesha wananchi kumiliki ardhi na kulima kwa mfumo ambao huduma zitatolewa kwa pamoja. Ujamaa wa Malaysia ulikuwa ni wa kumilikisha wananchi wao ardhi na kuwawezesha kuzalisha. Ujamaa wetu ulikuwa ni wa kumiliki kwa pamoja na hivyo kukosa uwajibikakaji. Badala ya kuboresha tunaona bora kwenda kwa wakulima wakubwa na kugawa ardhi hovyo bila mpango.
Hatuwezi kujifunza kwa wenzetu kweli? Lini tutaacha umazwazwa?
TAIFA LINA NYUFA
TAIFA LINA NYUFA
NDUGU KABWE Z. ZITTO, MB – BUNGENI TAREHE 6 MEI, 2013
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia leo katika mjadala huu muhimu sana.
Hapa Afrika kulikuwa kuna nchi, na bado ipo, inaitwa Ivory Coast. Ilikuwa ni nchi ambayo inasifika sana kwa amani na utulivu; na ilikuwa ni nchi ya kupigiwa mfano. Leo hii Ivory Coast imegawanyika vipande vipande. Ukienda leo Ivory Coast unakuta wanaoitwa Ivorite na wanaoitwa wageni ambao wazazi wao walienda Ivory Coast kufanya kazi miaka mingi sana. Lakini pili katika mgawanyiko huo kuna mgawanyiko mkubwa sana wa kidini kati ya watu wa Ivory Coast wanaotokea Kaskazini na watu wa Ivory Coast wanaotokea Kusini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa tuna Sierra Leone nchi ambayo wageni walikuwa wanakirimiwa katika hali ambayo haijawahi kutokea hapa duniani. Lakini leo Sierra Leone ina rekodi kubwa sana ya watu wenye ulemavu kwa sababu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe.
Naomba nichukue nafasi hii kufuatia matukio ambayo yametokea hivi karibuni na hasa jana na siku zilizopita ninanukuu hotuba ambayo Rais wa Awamu ya Tatu Mheshimiwa Benjamin Mkapa aliitoa katika Bunge hili tarehe 4 Novemba, 1998. Alisema:
“Mr. Speaker, after three years of my presidency, I can dare to modify the words of famous Zanzibar maestro Siti Binti Saada by saying, Tanzania is a good country, let one who wishes to come do so. God has showered blessings on our country. It is a country of unity, peace, love, rejoicing and exciding generosity. It is a country of people who love equality and justice. Our national unity brings from our firm believe in equality of human beings before God and before the Law. A Unity reinforced by correct policies of national building. Policies based on the principles of social justice, peace, harmony and development for all. A unity which is extra sensitive to policies, statements behavior and actions which may sore seeds discard hatred and suspicious among Tanzanians”
Mheshimiwa Mwenyekiti sitatafsiri. Lakini naomba kila Mbunge ajiulize leo iwapo Rais Mkapa tukimpa fursa ya kuja kuhutubia Bunge hili anaweza akayatumia maneno haya tena? Hakuna mtanzania yoyote anayeweza kuthubutu leo kutumia maneno haya tena kwa sababu nchi yetu ina nyufa. Ina nyufa ambazo kwa kujua au kwa kutokujua sisi kama watu ambao tumepewa wajibi na wananchi wa kuitunza nchi hii na kuipeleka pamoja tumejikuta tukiingia katika kutoa kauli, maneno na vitendo ambavyo ni “irresponsible” vinavyopelekea kugawanya nchi; na yanayotokea sasa ni matumizi ya nyufa hizo.
NDUGU KABWE Z. ZITTO
Asubuhi hapa Mheshimiwa Lissu amesema, ametoa rekodi ya namna ambavyo wanasiasa wa chama kinachoongoza (CCM) wamekuwa wakitoa kauli dhidi ya vyama vya upinzani kuhusiana na masuala haya ya kidini. Wametoa mfano kuhusu chama cha CUF kilipoitwa chama cha waislam, wamekitolea mfano kuhusu CHADEMA kinavyoitwa mpaka sasa chama cha wakristo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana ikawa ni rahisi sana tuka-“point fingers” kwa wenzetu nyie, ni rahisi sana; lakini CUF wakati wanaitwa ni chama cha waislam ambao walikuwa hawaitwi ni chama cha waislam hawakunyoosha mkono kupinga. Wakati CHADEMA kinaitwa cha cha Kikristo ambao hawaitwi hivyo hawakunyoosha mkono. Matokeo yakeni nini? Tumejenga hofu kubwa sana katika Taifa na hii ni lawama kwa wote. Wote kama nchi ili tuseme kwamba hapa tumekosea na tuanze upya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, adui anapokuja kwenye nyumba anaangalia ni wapi ambapo ni rahisi kamba kukatika. Tumeji-“expose”, tumejiweka wazi. Leo mtu anayetaka kuishughulikia Tanzania ata-deal na udini tu. Kwa sababu anajua watanzania hivi sasa wamegawanyika katika misingi hiyo. Jana limetokea tukio Arusha, angalia kwenye mitandao ya kijamii mara moja watanzania wenyewe kwa wenyewe na ukiangalia majina ya watu wanaojadiliana wanaanza kusemana kwa dini zao. Ndiyo hatari ambayo tumeifikia; na ndio anachokitaka adui. Ni hicho. Atakuja, wanaitwa “Agent Provacateur”, watapiga, mtabaki mnagombana ninyi. Tukiruhusu NYUFA hizi ziendelee hatutakuwa taifa. Ni lazima sote kwa pamoja tusimame imara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, waislam na wakristo nchi hii hawana chuki kwa sababu wanaishi pamoja, ni marafiki, ni ndugu na kama ingekuwa kwa mfano waislam wanawachukia wakristo waislam wangevunja makanisa au wangechoma makanisa au wangewalipua wakristo. Wakati wa tukio la Mwembechai ndipo ambapo Polisi waliingia mskitini wakaua watu, wanawake wakateswa kwenye magereza na kadhalika, watu wakakaa miezi mitano gerezani bila kushtakiwa lakini hapakuwa na mtukio yoyote ya namna hii. Waislam na wakristo wa nchi hii ni wamoja. Wananchi wetu ni wa moja lakini sisi viongozi kwa kutoa kauli ambazo ni “very irresponsible” tunawagawa watu wetu na ni lazima tukatae hali hii. Tunafanya nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima twende mbele. Kwanza ni lazima sasa Serikali ijenge utamaduni wa kufuatilia “grievances” zote ambazo wananchi wanazo bila kujali dini zao. Pili turuhusu watu kuwa huru kusema. Nimesikia hapa watu wanasema kwamba maandamano ni tatizo nakadhalika. Maandamano si tatizo, ukimzuia mtu kuandamana akiweka hasira zake kesho atafanya nini? Atatoka na bomu. Turuhusu “honest discussions” miongoni mwetu kama wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni lazima sasa tuseme ya kwamba ni marufuku kuwa na kauli za chuki “hate speeches”. Kama hatuna vipengele vya kisheria tutunge sheria kwa sababu kumekuwa na “hate speeches” nyingi sana katika hii nchi na hakuna hatua ambazo zinachukuliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, state, dola, ihakikishe inajiondoa kwenye shughuli za uendeshaji wa mambo ya kidini. Ijiondoe kabisa. Kwa mfano kuna lawama ya muda mrefu sana ya waislam kuhusu BAKWATA, Waislamu miaka mingi toka mwaka 1969 wakati Serikali imeunda BAKWATA wanalalamika. Leo hii Serikali ikitaka kuzungumza na waislam inafanya nini? Inaenda kuwaita BAKWATA. Hawana legitimacy ya waislam, hamtaweza ku-addres masuala ya waislam lakini ni rahisi sana kuweza kuongea na CCT kwa sababu CCT ni chombo ambacho kina uhuru wake. Kwa hiyo Serikali ijiondoe kwenye uendesheji wa shughuli za kidini. Hapa ndipo tutakapoweza kuhakikisha kwamba tunakuwa na nchi moja nchi ambayo ina amani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namaliza kwa kusema nchi hii si ya waislam peke yake, nchi hii si ya wakristo peke yake. Nchi hii si ya CCM au ya CHADEMA, CUF au ya NCCR-Mageuzi au TLP na kadhalika. Nchi hii ni moja, nchi hii ni ya Jamhuiri ya Muungano wa Tanzania. Lazima wote tusimame kuhakikisha tunailinda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru sana asante.
Mtwara : Serikali inavunja nchi kwa kutosikiliza Wananchi
Mtwara : Serikali inavunja nchi kwa kutosikiliza Wananchi
Kwa wiki ya tatu mfululizo kumekuwa na malumbano kuhusiana na suala la ujenzi wa Bomba la gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es Salaam. Kumekuwa na madai yenye nguvu ya hoja kutoka kwa wananchi wa Mtwara dhidi ya porojo kutoka kwa viongozi wenye dhamana ya kujibu madai haya ya watu wa Mtwara. Watu wa Mtwara kwa umoja wao na kwa kuungwa mkono na viongozi wa dini zote wamekuwa wakitaka Serikali ifikirie upya suala la mradi wa ujenzi wa Bomba la gesi na badala yake kujenga mitambo ya kufua umeme mkoani Mtwara na kusafirisha umeme huo kwenda maeneo mengine ya nchi. Kwenye moja ya maandishi yangu (Serikali iwasikilize watu wa Mtwara) nimeshauri kuwa Taifa liwe na gridi nyingine ya Taifa ambayo itatokana na Gesi tu na ianzie Mtwara.
Ikumbukwe kwamba katiba ya nchi, ibara ya 9 katika mabano J inataka mamlaka ya dola na vyombo vyake vyote kuhakikisha ya kwamba shughuli zote za kiuchumi zinaendeshwa kwa namna ya kwamba pasiwe mrundikano wa utajiri au shughuli za uzalishaji kwa watu wa chache. Katiba inaendela kwa kuelekeza kwamba uchumi wa nchi upangwe katika uwiano sawia (9, d). Watu wa Mtwara wanatekeleza matakwa haya ya katiba kwa kukataa mrundikano wa shughuli za kiuchumi wa nchi na utajiri wa nchi kua kwenye mikoa michache na hasa mkoa wa Dar-Es-Saalam.
Serikali imekuwa ikitoa majibu ya porojo na kuwatusi watu wa Mtwara na kama ilivyozoeleka Rais Jakaya Kikwete na Mawaziri wake wamekuwa wakisema suala la Mtwara linatumika na wanasiasa kujitafutia umaarufu. Inasikitisha sana kuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwaambia mabalozi wa nchi za kigeni waliopo hapa nchini kuwa yanayoendelea mkoani Mtwara yanachochewa na Wanasiasa tuliosimama na wananchi wanaodai haki ya kufaidi utajiri wa nchi yetu. Rais Kikwete na Mawaziri wake wameshindwa kabisa kuonyesha uongozi katika suala hili na hatimaye kuhatarisha umoja wa kitaifa.
Kwa udhaifu wa serikali na tabia ya kutafuta mchawi badala ya kutatua tatizo la msingi, wananchi wameendelea kukutana na hata wengine sasa kuanza kusambaza ujumbe wa kukata kipande cha nchi na kuanzisha Jamhuri ya Kusini. Nimeona kwenye mabango ya mkutano wa hadhara uliofanyika 19/1/2013 wananchi wakibeba mabango yanayoaishiria kuchoka kuwa sehemu ya Tanzania na kuanzisha Jamhuri ya Makonde kuanzia jiwe la Mzungu wilayani Kilwa mpaka mto Ruvuma. Haya yanatoka na kiburi cha Serikali kujishusha na kuwasikiliza wananchi wanao dai haki yao ya kikatiba.
Ni Serikali iliyokosa uhalali wa kutawala inayoweza kudharau hisia hizi za wananchi. Serikali ielewe kwamba kamwe haitaweza kulinda kila nchi ya bomba hili iwapo italijenga kwa nguvu. Badala ya kuzungumza na vyombo vya habari Serikali ifanye mazungumzo na wananchi wa Mtwara na kukubaliana na matakwa yao. Kitendo cha Serikali kung’ang’ania msimamo wake dhidi ya watu wa mtwara ni kitendo kinacho weza kuipasua nchi na hivyo kwenda kinyume na masharti ya katiba ibara ya 28 ambayo inasema: “kila raia ana wajibu wa kulinda uhuru wa nchi, uhuru mamlaka na umoja wa taifa.”ibara ya 28, 1.
Inawezekana Serikali inaogopa kuvunja makubaliano na Wachina ya mkopo wa dola za kimarekani 1.2 bilioni ambao imeuingia bila hata kushirikisha Bunge. Inawezekana Serikali na hasa watendaji wa Serikali waliojadili mkopo huu wameshapata chao na hivyo kuogopa kusikiliza madai halali ya wananchi. Lakini yote hayo hayawezi kuwa zaidi ya Umoja wa nchi yetu. Hatuwezi kukubali nchi yetu ipasuke vipande vipande kwa sababu tu ya kulinda mkataba wa bilioni 1.2 tuliokopa China, ambayo serikali inang’ang’ania.
Tunafahamu kwamba ubalozi wa China umeandika barua serikalini kuwaondoa raia wa China waliopo Mtwara kwa hofu ya maisha yao. Serikali inaficha ukweli huu kama ilivyoficha ukweli kwamba Naibu Waziri wa Nishati na Madini bwana George Simbachawene alifukuzwa na wananchi wa Mtwara alipokwenda hivi majuzi. Serikali itaficha ukweli mpaka lini? Lazima tupate majawabu.
Kwanza Serikali iweke wazi mkataba wa ujenzi wa Bomba hili. Kamati ya Bunge ya POAC ilipokuwa inapitia mahesabu ya TPDC iliomba mkataba na kwa mshangao mkubwa wabunge wakaambiwa Mkataba haupo TPDC bali upo Wizarani. Kwa nini Mkataba huu wa matrilioni ya Fedha unafichwa? Mkataba huu ulisainiwa pamoja mikataba mingine 2, mmoja wa kujenga nyumba za wanajeshi wa thamani ya dola za kimarekani 400 milioni na mwingine wa mawasiliano jeshini wa dola za kimarekani 110 milioni, na mikataba yote mitatu imesainiwa kimya kimya bila kushirikisha wananchi kupitia Bunge. Lazima mikataba yote hii iwekwe wazi.
Pili, Mkataba huu uchunguzwe kama unalingana na thamani ya fedha maana kwa utafiti wa awali inaonyesha kuwa bei ya ujenzi wa bomba imepandishwa maradufu. Wastan wa kujenga bomba la gesi duniani ni dola za kimarekani 1.2 milioni kwa maili moja. Mradi huu wa Tanzania utagharimu dola za kimarekani 2.2 milioni kwa kilomita moja (maili 1 ni sawa na kilomita 1.6).
Tatu, Serikali ibadilishe Mkataba huu kuwa wa mkopo wa kujenga Mitambo ya kufua umeme Mtwara na ujenzi wa Msongo wa Umeme kama gridi ya pili ya Taifa. Kwa sasa Tanzania ina gridi moja ambayo inabebwa na bwawa la Mtera linalo tegemea mto Ruaha ambao hivi sasa unakauka miezi 5 katika miezi 12 ya mwaka. Ni dhahiri kwamba kwa usalama wa Taifa na hata kwa gharama Nchi itafaidika zaidi kwa kujenga gridi nyingine kutokea Mtwara badala ya kusafirisha gesi kuja Dar-Es-Salaam.
Serikali haitashinda vita hii kwa kuzusha kwamba ama wanasiasa wanaopinga wanatumika na makampuni mengine au kwa mataifa ya magharibi kutaka kuvuruga nchi. Serikali ijitazame yenyewe. Bila kufanya hayo tunayo pendekeza hapo juu, wananchi wataendelea kupigania hako yao. Hii ni vita ya uwajibikaji. Wananchi wanataka kufaidika na rasilimali za nchi yao. Kwa vyovyote vile upande wa wananchi utashinda. Vita ya uwajibikaji kwenye rasilimali za nchi sio ya vyama vya siasa, ni vita ya wananchi. Chama cha siasa kitakachokwenda kinyume na matakwa ya wananchi, kinajichimbia kaburi.