Zitto na Demokrasia

Zitto na Demokrasia

Archive for the ‘Posho za Vikao’ Category

Mahojiano ya Zitto Mlimani Tv(Keki ya Taifa) kuhusu Posho za Wabunge

with 4 comments

Mahojiano MlimaniTV Part 1

Mahojiano MlimaniTV Part 2

Mahojiano MlimaniTV Part 3

Mahojiano MlimaniTV Part 4

Written by zittokabwe

December 17, 2011 at 10:52 AM

Msimamo wangu: Kupandisha posho za wabunge ni ukichaa na kutojali Hali ya Nchi

with 15 comments

Nimeshtushwa sana na taarifa za kupandishwa kwa posho za vikao kwa Wabunge. Nimeshtushwa zaidi kwamba Posho hizi zimeanza kulipwa katika mkutano wa Bunge uliopita kabla hata Rais hajaamua maana maslahi yote ya Wabunge huamuliwa na Rais Baada ya kupokea mapendekezo ya Bunge kupitia Tume ya Bunge.

Wabunge wote watambue kwamba kuamua kujipandishia posho zao bila kuzingatia Hali ya maisha ya mwananchi wa kawaida ni usaliti usio na mfano. Mbunge yeyote ambaye anabariki Jambo hili au anaishi hewani haoni tabunza wananchi au ni mwizi tu na anaona Ubunge ni Kama nafasi ya kujitajirisha binafsi.

Kwa Wabunge wa Chadema, wajue uamuzi kuhusu posho ni uamuzi wa chama na ni uamuzi wa kisera. Mbunge yeyote wa Chadema anayepokea posho za vikao anakwenda kinyume na maamuzi ya sera za chama tulizoahidi wananchi wakati wa uchaguzi. Nimemwomba Katibu Mkuu wa chama kuitisha kikao maalumu cha Kamati Kuu ya chama kujadili suala hili.

Toka tarehe 8 juni mwaka 2011 nilikataa kupokea posho za vikao. Popote ninapohudhuria vikao huomba Risiti ya fedha ninazokataa. Baadhi ya Wabunge Kama Januari Makamba wamekataa posho na hata kwenye semina ya kamati ya nishati alikataa na tumeona kwenye vyombo vya habari jina lake likiwa limekatwa ilhali viongozi wakubwa kabisa wamechukua posho. Nampongeza kijana mwenzangu kwa uzalendo huu. Nawataka wabunge wengine wenye Moyo wa dhati kukataa sio tu ongezeko hili la posho Bali posho yote ya vikao. Kwa nini mbunge akubali kulipwa kwa kukaa?

Tazama nchi hii, juzi serikali ilipokea Msaada wa tshs 20bn kwa ajili ya Sensa ya mwakani wakati wabunge wanalipwa 28bn Kama posho za kukaa tu.

Tanzania inaagiza gesi ya matumizi ya nyumbani kutoka nje kwa kutumia mamilioni ya dola za kimarekani. Kuwanda cha kutengeneza LPG kinagharimu tshs 35bn tu, Wabunge peek Yao kwa mwaka wanatumia 28bn kwa posho za kukaa tu achilia mbali mishahara na marupurupu mengine.

Ipo siku Watanzania watatupiga mawe kwa usaliti huu dhidi yao.

****

June 10, 2011-Barua: Posho za Vikao

Update: Posho za Vikao- Majibu ya Ofisi ya BUNGE na Uamuzi Wangu (June 11, 2011)

June 19, 2011- SUALA LA POSHO ZA VIKAO: WAZIRI MKUU-ANAPASWA KUCHUKUA HATUA MBILI, AFUKUZWE AU AJIUZULU!

October 10, 2011-#1 Say NO to Posho!

October 14,2011-#2 Say NO to posho!

Written by zittokabwe

November 28, 2011 at 10:29 AM

Posho za wabunge zapanda kimyakimya

with 8 comments

ZAPANDA KUTOKA SH70,000 HADI 200,000, NI ZAIDI YA ASILIMIA 150
Fredy Azzah

Bunge Letu

HUKU mjadala wa kufutwa au kwa posho za wabunge na watumishi wengine wa Serikali ukiwa umefifia, posho za vikao (sitting allowance) za wabunge zimepanda kutoka Sh70,000 kwa siku hadi Sh200,000, imefahamika.

“Zimeongezeka kutoka Sh70,000 mpaka 200,000, wameanza kulipwa Bunge lililopita hili ni ongezeko la karibu mara tatu, yaani asilimia 154,” kilieleza chanzo chetu kutoka ndani ya Ofisi za Bunge.

Kutoka na ongezeko hilo, kwa sasa kila mbunge atakuwa akilipwa Sh80,000 ikiwa ni posho ya kujikimu (perdiem) anapokuwa nje jimbo lake, posho ya vikao (sitting allowance) Sh200,000 na mafuta ya gari Sh50,000 kila siku, ambazo jumla yake ni Sh330,000 kwa siku.

Kutokana na ongezeko hilo, Bajeti ya Bunge kwa ajili ya posho za vikao vya wabunge imepanda na kufikia Sh28 bilioni kwa mwaka.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alipoulizwa kuhusu taarifa hizo alisema hawezi kuzungumzia jambo hilo kwa sababu siyo msemaji wa wabunge, bali Ofisi ya Bunge.

“Ni nani kawapa hizo taarifa bwana, au ni vyanzo vyenu vya habari?” alihoji Dk Kashililah.

Baada ya kuelezwa kuwa taarifa hizo zimetoka kwenye vyanzo vyetu vya kuaminika alisema “Hao wana utaratibu wao bwana, labda mtafute Spika ndiye msemaji wa Wabunge.”

Juhudi za kumpata Spika, Anne Makinda kutoa ufafanuzi wa suala hili, hazikufanikiwa baada ya simu yake kuita wakati wote bila kupokewa hata pale alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu (sms) hakujibu. Hata simu zote za Naibu wake, Job Ndugai hazikupatikana.

Hata hivyo, Mbunge wa Ludewa (CCM), Deo Filikunjombe alisema kuongezeka kwa posho hizo kunatokana na wabunge kuwa wanalipwa mishahara midogo kulingana na kazi wanayofanya.

Alisema endapo wawakilishi hao wa wananchi wangekuwa wanalipwa mishahara inayolingana na kazi wanayofanya, kusingekuwa na sababu ya kuongezeka kwa posho hizo.

“Ninachosema mimi, siyo wabunge peke yao, lakini watumishi wote wa umma wanalipwa mishahara midogo sana mimi binafsi sitegemei posho za Bunge, kabla ya kuingia bungeni nilikuwa nimefanya kazi kwa miaka 14 na nilikuwa napata mshahara mzuri tu,” alisema Filikunjombe.

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alisema amezisikia taarifa hizo za kuongezeka kwa posho lakini siyo kwa undani. Hata hivyo alisema hakuwa katika nafasi nzuri ya kuzungumza suala hilo.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema walivyokuwa wakipinga posho hizo wakati zilivyokuwa Sh70,000 waandishi wa habari walichukua suala hilo kama ajenda ya Chadema, hivyo kupandishwa kwa posho hizo ni matokeo ya watu kuwapuuza walivyokuwa wakizipinga.

“Msimamo wetu sisi tulishautoa tangu wakati posho zikiwa Sh70,000 wakati sisi tukipinga hizi posho waandishi wa habari na Watanzania mlichukulia suala hili kama ajenda ya Chadema, sisi wenyewe tupo wachache bungeni, tulichotaka ni kuonyesha jinsi fedha za Watanzania zinavyotumika vibaya,” alisema na kuongeza:

“Achilia mbali hizo 200,000 za wabunge kuna watu huko serikalini wanalipwa mpaka Sh400,000 au Sh1 milioni kwa siku nyie ulizeni.”

Alipoulizwa kama amechukua posho hiyo ya Sh200,000 alisema hajafanya hivyo kwa sababu hazifuatilii.

“Sijui hata kama zimeanza kulipwa au la kwa sababu huwa sizifuatilii na haka kama suala la posho hilo zilijadiliwa wakati wa vikao vya mwanzo mimi sikuwepo kwa sababu tulikuwa kwenye kesi yetu Arusha na bungeni tulikuja mwishoni wakati wa Muswada wa Katiba,” alisema Mbowe.

Ongezeko hili la posho za wabunge limekuja wakati Watanzania wakiendelea kuishi kwenye maisha magumu yanayochangiwa na mfumuko wa bei ambao mpaka mwisho mwa Oktoba ulikuwa umefikia asilimia 17.9.

Pia ongezeko hili limekuja wakati Watanzania wakiwa na matumaini ya posho hizi kupunguzwa baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutangaza bungeni kuwa Serikali imekubali pendekezo la kutafakari na kuziangalia upya posho mbalimbali wanazolipwa wabunge na watumishi wote umma.

Mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali alisema kuwa hawezi kuzungumza chochote juu ya posho hizo kwa kuwa hajapata barua rasmi juu ya kupanda kwake.

“Sijapata barua yoyote, nikiuliza na kupata majibu kwa wahusika nitakuwa na uhakika na nitakupa maoni yangu na msimamo wangu vizuri kabisa, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote,” alisema Mkosamali.

Juni 7, mwaka huu Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Zitto Kabwe, aliwasilisha barua Ofisi ya Bunge akikataa posho akisema watumishi wa Serikali na wabunge, hawastahili kulipwa posho wanapohudhuria vikao rasmi vya uwajibikaji wao wa kawaida.

Zitto alisema posho hiyo haistahili kulipwa kwake, wabunge wengine wala watumishi wa umma kwa kuwa kuhudhuria vikao ni sehemu ya kazi zao.

Alisema kitendo cha Waziri Mkuu kueleza kuwa watatafakari na kuangalia upya na kwamba suala la posho ni sera ya taifa na Ilani ya Uchaguzi ya CCM, ni ishara ya kiongozi huyo wa juu kukubali wazo la Chadema na safari ya kufuta posho hizo.

Awali, mara baada ya Chadema kutangaza msimamo huo, Spika Makinda alipinga uamuzi wa kususia posho akisema suala hilo lipo kisheria na kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kuamua kuliondoa.

Alisema wabunge wa Chadema wataendelea kulipwa posho za vikao kupitia akaunti zao za benki na watatakiwa kusaini fomu ya mahudhurio ya Bunge, vinginevyo watajiweka katika wakati mbaya.

Hata hivyo, akihitimisha hoja za wabunge katika hotuba yake ya makadirio ya matumizi ya ofisi yake na zilizo chini yake juzi, Pinda alisema suala la posho lipo kwenye mchakato wa kuangaliwa upya.

Source: Mwananchi

Written by zittokabwe

November 28, 2011 at 9:38 AM

MPs sitting allowance up 185pc

with 2 comments

By The Citizen Reporter
Dar es Salaam. The daily sitting allowance for an MP has been increased by more close to over 285.7 per cent, The Citizen has been reliably informed.

Our Parliament

Some sources who attended the just-ended fifth Parliament told this paper that the amount has gone up by almost three times –  from Sh70,000 to a whopping Sh200,000 per day.

The latest adjustment has effectively increased the amount of cash that goes to a legislator pocket daily during a Bunge session to Sh330,000 because, besides the Sh200,000 for sitting, they also receive a per diem of Sh80,000 plus Sh50,000 for fuel.

However, when contacted, Clerk of the National Assembly Thomas Kashillila said his office was not aware of the said increase.

“I understand there was talk among MPs to have their allowances raised, but if that has been effected, my office hasn’t been formally informed yet.

Therefore, I cannot confirm that MPs’ allowances have gone up,” he said over his mobile phone yesterday. Dr Kashillila advised The Citizen to check up with the Speaker of the National Assembly Anne Makinda or her deputy, Mr Job Ndugai, for a precise response but our efforts were in vain for the two officials’ phones were not reachable despite repeated attempts.

Though many MPs who attended the just- ended Parliament session were hesitant to comment on the matter, impeccable sources confirmed to this paper that the sitting allowances have nearly tripled.

The MPs’ hesitation to comment on the raise could be on account of uneasiness stemming from the recent debate in which the opposition Chadema pressed for abolition of sitting allowances for the lawmakers.

When contacted, the Leader of Official Opposition in the Parliament, Mr Freeman Mbowe, saidthe latest raise clearly showed that the government has not taken note of Chadema’s sentiments over allowances.

He maintained that his party’s stand over allowances should not be personalised as it was national resources that are being used to overpay a few individuals while the majority of Tanzanians languished in abject poverty.

“We abide by our stand since the time the daily sitting allowances stood at Sh70,000. When we issued statements contending the allowance, some people, and a section of the media took the issue as a Chadema agenda, but we wanted to expose the misuse of taxpayers’ money,” he said adding:

“We have MPs’ pocketing Sh200,000 as sitting allowance and then there are some people in the government who are paid between Sh400,000 and Sh1 million as daily allowance.”

Mr Mbowe said personally, he would not know for certain that there has been a rise in sitting allowances for MPs since he doesn’t collect his.

“Maybe the new allowances were discussed in the House at the time I was attending  my cases in Arusha… I was only present during a few sessions towards the end of the debate on the Constitutional Review Act Bill,” he said.

The increase in MPs’ allowance comes at a time when the majority of ordinary Tanzanians are lamenting over the cost of living against their frozen incomes. Hardships for the mwananchi are reflected on the two-digit inflation which at the moment stands at around 17.9 per cent as announced by the National Bureau of Statistics (NBS) recently. The decision to increase MPs’ sitting allowance is also said to contradict the government’s five years development plan, unveiled mid this year, one of whose agenda was to reduce allowances.

Prime Minister Mizengo Pinda is also on record as telling the Parliament during the Budget session that the government had agreed to a proposal to slash allowances.

When contacted, Felix Mkosamali (Kibondo-NCCR Mgeuzi) and Rev Peter Msigwa (Iringa Urban – Chadema) declined to discuss the matter in detail and said MPs have not been officially informed of the decision to increase their sitting allowances. “I have not received any letter informing me that my allowance has been increased. I will inquire and once I get a categorical answer I will make my stand over this issue known,” said Mr Mkosamali.

But Deo Filikunjombe (Ludewa-CCM) said the raised allowance was justifiable given the meagre salaries paid to lawmakers.

“And my stand is that if MPs were being paid in accordance with the weight of their job, there would be no need to pay them hefty allowances and this is not for MPs only. Civil servants too receive very small salaries,” he said.

In June this year, the Deputy Leader of the Opposition in the Parliament, Mr Zitto Kabwe, presented a letter in which he rejected his sitting allowance on the grounds that MPs were not supposed to be paid for sitting, arguing that their job, for which they receive monthly salaries, is to sit at the Bunge and debate.

Mr Kabwe’s stand, however, drew stiff opposition from a majority of the MPs, including some from his own party.

Source: The Citizen

Written by zittokabwe

November 28, 2011 at 9:33 AM

SUALA LA POSHO ZA VIKAO: WAZIRI MKUU-ANAPASWA KUCHUKUA HATUA MBILI, AFUKUZWE AU AJIUZULU!

with 6 comments

Kwanza nasikitika kuwa Waziri Mkuu amerejesha suala la posho za vikao kwenye mjadala ilhali lilimalizwa baada ya Bungekupitisha Mpango wa maendeleo wa miaka 5.  Kitendo cha Waziri Mkuu kulilia posho kinaonyesha jinsi asivyo tayari kusimamia na kutetea sera za serikali anayoongozwa. Anapaswa kuchukua hatua mbili, ama afukuzwe kazi kwa kwenda kinyume na maamuzi ya kisera ya serikali yaliyopitishwa na baraza la mawaziri na Bunge, au ajiuzulu. Hatuwezi kuvumilia viongozi wanaokwenda kinyume na sera za serikali.

Waziri Mkuu: Mizengo Pinda

Written by zittokabwe

June 19, 2011 at 6:12 PM

Update: Posho za Vikao- Majibu ya Ofisi ya BUNGE na Uamuzi Wangu

with 16 comments

MAJIBU YA OFISI YA BUNGE

View this document on Scribd

 

UAMUZI WANGU-MAJIBU KWA OFISI YA BUNGE

View this document on Scribd

Written by zittokabwe

June 11, 2011 at 8:31 AM