Archive for the ‘CUF’ Category
Zitto ‘amgeuzia kibao’ CAG(Gazeti la Mwananchi)
RUZUKU VYAMA VYA SIASA
*ADAI AMESHINDWA KUKAGUA SH83 BILIONI
Kizitto Noya
WAZIRI Kivuli wa Fedha na Uchumi, Zitto Kabwe ametaka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ichunguzwe kwa uzembe wa kushindwa kukagua hesabu za ruzuku za vyama vya siasa kwa muda wa miaka mitatu.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Kabwe alisema CAG ameshindwa kukagua ruzuku ya Sh83 bilioni iliyotolewa kwa vyama vya siasa nchini tangu mwaka 2005 hadi 2010.
Alisema ingawa kuna tatizo katika Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, CAG hawezi kumtupia mzigo huo pekee yake kwani naye anahusika.
“Nikiwa Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, ninamwomba CAG afanye audit (ukaguzi) kwa vyama vyote vya siasa kwa miaka mitatu iliyopita sasa na siyo baada ya miezi sita,” alisema Kabwe na kuongeza:
“Ruzuku ya vyama vya siasa ni eneo ambalo huwa haliangaliwi kabisa na fedha nyingi ya walipa kodi inakwenda katika vyama. Kuanzia mwaka 2005 mpaka 2010 jumla ya Sh 83 bilioni zimetolewa kama ruzuku kwa vyama vya siasa,” alisema Kabwe na kuongeza:
“Fedha zote hizi kwa miaka yote hii, hazikuwa zinakaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, (CAG).”
Kwa mujibu wa Kabwe, ubadhirifu unaoweza kujitokeza kwenye fedha za ruzuku zinazotolewa kwa vyama vya siasa, unatokana pamoja na mambo mengine na CAG kushindwa kukagua ruzuku hizo tangu vyama vianze kuipata mwaka 1996.
“Ndiyo maana kumekuwa na ubadhirifu mwingi wa fedha za ruzuku kwenye vyama takriban vyote hapa nchini,” alisema Zitto.
Alisema mwaka 2008, alipeleka pendekezo la mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa katika Bunge la Novemba kutaka vyama vikaguliwe na CAG.
Alisema pendekezo lake lilisomeka: “Vyama vyote vitakaguliwa na CAG na itakuwa ni jukumu la vyama vya siasa kupeleka taarifa zao kwa CAG kwa mujibu wa sheria.”
“Hivyo tangu mwaka 2008 vyama vinatakiwa vikaguliwe na CAG kwa mahesabu yao lakini mpaka sasa hakuna chama ambacho kimeshakaguliwa,” alisema Zitto na kuongeza:
“CAG mwaka huu amelalama tu kwenye taarifa yake kuwa vyama havikupeleka taarifa zao kwa Msajili. Ametoa miezi sita ili wasahihishe makosa? miezi sita ili watafute nyaraka za kugushi ili kuyaweka mahesabu sawa?” alihoji.
Kabwe alisema kauli ya CAG kwamba hahusiki kuvikagua vyama vya siasa ni kukwepa majukumu kwani sheria ya sasa inamtaka afanye hivyo kwa kuteua wawakilishi.
“Hakuna sababu kwa CAG kutoa miezi sita kwa vyama, bali vyama sasa viheshimu Public Audit Act,(Sheria ya Ukaguzi wa Fedha za Umma), Public Finance Act (Sheria ya Fedha za Umma) and (na) Political Parties Act (Sheria ya Vyama vya Siasa)”
Kwa mujibu wa Kabwe, CAG anapaswa kudai mahesabu kutoka kwa vyama na wala si kusema kuwa hahusiki na watu binasi. “Vyama siyo ‘individuals’, vyama ni taasisi,” alisema.
“Kwa sheria mpya, wakaguzi wa vyama wanapaswa kuteuliwa na CAG na siyo vyama kwenda kuokota wakaguzi na kuweka hesabu zao kama ambavyo imezoeleka,” alisema.
Zitto alisema vyama vya siasa ndivyo vinavyounda Serikali, hivyo iwapo haviheshimu fedha za walipa kodi, Serikali wanazounda haziwezi kuheshimu fedha za walipa kodi.
“Ruzuku iliyotolewa kwa vyama mwaka 2010 ilikuwa ni mara tatu ya Bajeti ya Wizara ya Afrika Mashariki au ni zaidi ya Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara. CAG ni lazima afanye kazi yake,” alisema na kuongeza:
“Msajili wa Vyama naye achunguzwe, ofisi yake inafanya kazi kwa mujibu wa sheria, kwa nini hakuwa na taarifa za vyama vya siasa wakati yeye ndiye mwenye jukumu la kusimamia vyama.”
“Iwapo anashindwa kusimamia ruzuku kukaguliwa atawezaje kusimamia matumizi ya fedha kwenye uchaguzi wakati uchaguzi uligubikwa na matumizi ya fedha nyingi za kifisadi,” alidai Zitto.
Ripoti ya CAG iliyoishia Juni 30 mwaka 2010, imeeleza kuwa vyama sita vyenye wawakilishi bungeni vimeshindwa kuonyesha taarifa za matumizi ya ruzuku ya Sh17.14 bilioni.
Vyama hivyo ni CCM, CUF, Chadema, NCCR-Mageuzi, TLP na UDP. Katika hesabu za kawaida kuhusu fedha hizo, chama hicho tawala kimepata mgawo wa Sh12 bilioni kutokana na asilimia 70 ya mgawo.
CUF kinachopata asilimia 20 ya ruzuku kimepata mgawo wa Sh3.43 bilioni, Chadema chenye asilimia nane Sh1.37 bilioni na vyama vitatu vinavyoshikilia asilimia mbili Sh343 milioni.
Akijibu Madai hayo, Utouh alisema: “Sijakwepa majukumu. Fedha zinatoka serikalini, zinakwenda kwa Msajili wa Vyama.”
“Yeye (Msajili), ndiye mwenye kazi ya kuvigawia vyama fedha hiyo na sheria inataka baada ya matumizi, vyama vinapaswa kutengeneza hesabu zake na kuziwakilisha kwa Msajili. Siyo kazi yangu kuvitengenezea mahesabu vyama vya siasa.”
Kuhusu madai ya Zitto kwamba utaratibu huo wa Msajili kukagua vyama uko kwenye sheria ya zamani ambayo Zitto alidai kwamba alishatoa mapendekeza bungeni na kufanyiwa marekebisho, yanayomtaka CAG kuteua wakaguzi wa hesabu za vyama vya siasa, Utouh alisema:
“Mwulize yeye (Zitto) chama chake kilishanipelekea mahesabu ili niyakague kama anajua hivyo ndivyo inavyotakiwa? Tupo hapa kufanya kazi. Hatupo kukwepa majukumu. Mwulize kama hivyo ndivyo sheria inavyotaka Chadema ilishawahi kuniletea mahesabu yake?”
Chanzo: Gazeti la Mwananchi
Do MPs who speak out in Parliament get re-elected?
Uwazi at Twaweza has released a new policy brief titled, Who returned? Performance in the Bunge and MP re-election. The brief shows that ordinary MPs reelected in 2010 were more active than their counterparts who were not reelected. It also analyses results by political party affiliation. The brief is based on information available on the Bunge website (www.bunge.go.tz). Read the full brief here to know six key facts about what increases an MP’s chances for re-election.
Source: Uwazi at Twaweza
Tamko: Kuhusu Habari ya Gazeti la Sunday Citizen-Tarehe 20-Machi-2011
Salaam,
Naomba nitumie nafasi hii kufafanua kuhusu habari ya gazeti la Sunday Citizen ya Tarehe 20-03-2011.
Nyote mnafahamu kwamba mkutano wa pili wa Bunge la kumi ulikutana kwa ajili ya kuchagua wenyeviti wa Kamati za Bunge ili kupata Kamati ya Uongozi ya Bunge.
Mimi niligombea uenyekiti wa kamati ya POAC kamati niliyokuwa nikiongoza toka Bunge la kumi. Kwa mujibu wa kanuni za Bunge kamati za oversight ni kamati za Kambi rasmi ya upinzani Bungeni ambapo CHADEMA ilitimiza masharti yote ya kuwa kambi rasmi ya upinzani Bungeni.
Wabunge wa CCM kwa kushirikiana na CUF, NCCR na UDP waliamua kuikomoa chadema kwa kuinyima kamati hizi na hivyo kufanya tafsiri ya kanuni. Habari ambazo tulizipata ni kwamba kamati ya PAC ingekwenda kwa Cheyo, LAAC kwa Mrema na POAC kwa Hamad Rashid na hivyo chadema kutopata nafasi yeyote na kupunguza nguvu yake kwenye kamati ya uongozi ya Bunge ambayo hupanga ajenda za Bunge.
Mara baada ya kupata majina ya wajumbe 15 wa kamati ya POAC nilianza kampeni na msaidizi wangu kwenye kampeni alikuwa ni Mhe. Regia Mtema. Tuligawana wabunge ili kupata kura 8 ambazo zingehakikisha ushindi. Kati ya kura hizo nane, tatu ni zetu sisi wabunge wa CHADEMA-Mimi, Mhe Matiko na Mhe Mtinda. Kwa hiyo nilikuwa natafuta kura 5 kutoka CCM. Spika alipotangaza majina ya wajumbe jina la Hamad Rashid halikuwemo.
CCM wakaitisha kikao cha caucus yao ili kufanya maamuzi juu wenyeviti wa kamati (walifanya hivyo hivyo wakati Mimi na Dr. Slaa tulipochaguliwa kuwa Wenyeviti mwaka 2008). Kikao chao kikaamua kwamba mwenyekiti awe Hamad Rashid, na kwa kuwa yeye sio mjumbe basi Spika amteue kuwa mjumbe. Kama Spika hatamteua basi Mhe Amina Mwidau wa CUF(Viti Maalum kutokea Tanga) achaguliwe. Wajumbe wa kamati ya POAC kutoka CCM wakapinga ndani ya kikao chao kwamba mimi ninafaa zaidi kuliko huyu Mhe.Amina Mwidau wa CUF (ambaye mie wakati huu nilikuwa simfahamu kabisa).
Wajumbe wote waliopinga uamuzi wa chama ninaambiwa walizomewa na hatimaye kuitwa jina mmoja kutamka kuwa watafuata uamuzi wa chama. Pinda ndiye aliongoza kikao hicho.Spika alipoambiwa abadili orodha yake na kumweka Mhe Hamad Rashid, alikataa kwa hoja kwamba orodha imeshakuwa public na hawezi kuibadili.
Akabakia Mhe Mwidau kama mgombea ambaye CCM wanamtaka. Wajumbe watano ambao walikuwa wamenihakikishia kura walimfuata Waziri Mkuu kumwambia kuwa wao wataenda kinyume na maamuzi ya chama na watanipigia kura.
Usiku kucha wa siku ya kuamkia kupiga kura mimi na Regia tulizunguka kuhakikisha kura zetu zinabakia intact na hata kumshawishi Mbunge wa CUF Mwidau ajitoe. Tukiwa tunajiandaa kwenda kwenye kupiga kura CCM wakaitwa kwa dharura na kuambiwa na Pinda kuwa uamuzi wa jana usiku umefutwa na Rais ameagiza achaguliwe Zitto. Tukaenda kwenye uchaguzi, nikagombea na Mhe Mwidau na nikapata kura 13 dhidi ya 2 za Mwidau. Hiyo ndio background kwa ufupi.
Kwa hiyo, sikumpigia simu Rais kutaka anisaidie. Nimekaa bungeni miaka mitano na nazijua siasa za Bunge. Nilikuwa nimejipanga kiasi ambacho kushindwa kungetokea iwapo tu Chief Whip wa CCM angekuja kusimamia mwenyewe uchaguzi. Ikumbukwe pia mie nimekuwa student leader, najua siasa za kipiganaji. Inawezekana hata huyo mgombea angekuja kwenye mkutano baada ya kura kupigwa!
CCM walibadili msimamo baada ya kutishiwa strong rebellion from their own ranks that they will vote for me. Wabunge 5 wa CCM kati ya 11 kumwambia Pinda kuwa watanipa mimi kura ilikuwa ni ishara tosha kwamba wanaweza kuaibika.
Pia inawezekana kabisa CCM walibadili msimamo asubuhi ili kutaka kudhoofisha hoja ya chadema kwamba mabadiliko ya kanuni yaliwalenga kwa kusema ‘mbona Zitto kashinda’ Hayo ndio maelezo ninayoweza kuwapa ndugu zangu kuhusiana na suala hili. Kama kuna maswali zaidi nitawajibu kwa kadiri ya uwezo wangu.
Zitto Kabwe (MB)
20/03/2011
The results of the opinion polls/Utafiti wa Synovate
The results of the opinion polls conducted by Synovate Tanzania in May 9th-19th 2010.
Hii hapa(Download)