Archive for the ‘chadematv’ Category
Siku ya 9 ya Ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi – Jimbo la Igunga, Wilaya ya Igunga
Siku ya 9 ya Ziara ya CHADEMA kanda ya Magharibi imetufikisha Jimbo la Igunga, Wilaya ya Igunga.
Tumefanya mikutano 6 katika kata sita tofauti, tumefungua matawi ya chama na kuhutubia wananchi. Pia tumepokea kero za wananchi zinazowakabili katika maisha yao ya kila siku.
Tukiwa Katika kata ya Choma tumeshuhudia kiwanda cha kuchambua Pamba kilicho binafsishwa kikiwa kimetelekezwa na mwekezaji toka mwaka 1998. Ginnery hii iliyokuwa mali ya umma na kuajiri wafanyakazi 500 kwa shifti 3 kila siku (jumla 1500) nyakati za msimu imekufa na baadhi ya Mashine kuuzwa kama chuma chakavu. Kijiji cha Choma kimedorora kiuchumi kutokana na ubinafsishaji huu. Nimewaeleza wananchi kuwa nitafuatilia suala hili la Ginnery ya Manonga, katani Choma na kuwajulisha hatua mwafaka za kuchukua.
Nimependekeza pia kwamba iwe marufuku kuuza nje mazao ghafi kwani tunakuwa tunauza ajira za watu wetu. Suala hili nimekuwa nikilisema Bungeni mara kwa mara kwamba ni lazima kusafirisha mazao yaliyoongezwa thamani kwa kupiga marufuku kuuza korosho ghafi, Pamba ghafi, kahawa ghafi na Katani ghafi. Viwanda vya kilimo vinaongeza ajira sana kwa wananchi na ni suluhisho endelevu kwa tatizo la ajira na kuondoa umasikini.
Niliwapa mfano wa kiwanda kilichouzwa huko mtwara na kugeuzwa godown la kuhifadhi korosho na godown liligeuzwa kuwa kiwanda cha kubangua korosho! Niliwaeleza namna viongozi wa Serikali wanavyochanganya dhana ya uhuru wa biashara (liberalisation) na ubinafsishaji (privatisation). Dhana mbili zinazochanganya watawala wengi wa Afrika na kujikuta wakiuza mali za umma kiholela. Unaweza kuwa na Mashirika ya Umma yakishindana katika soko na makampuni binafsi. Ubinafsishaji holela unatengeneza ‘private monopolies’ na kuathiri sana ukuaji wa uchumi kutokana na ufanisi mdogo ie efficiency.
Nimerejea wito wangu wa kutaka sera ya hifadhi ya jamii kwa wakulima kupitia vikundi vyao na ushirika. Nimesisitiza umuhimu wa kuweka akiba ili kuongeza uwekezaji wa ndani na hasa uwekezaji wa miundombinu ya kilimo. Nimeonya tabia ya wananchi kukimbilia kulipwa fidia badala ya kutaka kushiriki katika miradi mikubwa ya kilimo. Kilimo endelevu ni kilimo cha wakulima wadogo wanapata huduma pamoja (integrated production schemes) badala ya wakulima wakubwa wenye kuhitaji manamba. ‘outgrower’s schemes’ ndio mwelekeo sahihi kuwafanya wananchi wamiliki ardhi, wawe na ushirika imara, wawe na hifadhi ya jamii na waondokane na umasikini.
Leo nikiwa kijijini Choma na mjini Igunga nimewaambia wananchi umuhimu uwazi wa mapato ya viongozi wa umma. Nimewaambia kuwa mishahara ya viongozi wa umma haipaswi kuwa siri na inapaswa kukatwa kodi. Kama nilivyoahidi niliokuwa mjini Mpanda, nimewaambia kuwa mshahara wa Rais wa Tanzania ni Tshs 384m kwa mwaka. Kipato hiki hakikatwi kodi na Rais hupata huduma mbalimbali bure. Niliahidi kwamba kwa kuwa gazeti la Mwananchi lilifungiwa kwa sababu ya kutaja mishahara ya watumishi wa Serikali, basi ni vema kuonyesha Serikali kuwa lile sio kosa na wananchi wana haki ya kujua. Ndio maana nikachukua hatua ya kutaja kipato cha Waziri Mkuu na Rais.
Nimemaliza awamu ya kwanza ya ziara ya kanda ya Magharibi. Nimetembelea jumla ya kata 53 katika majimbo 10 ya uchaguzi ya mikoa ya Katavi na Tabora. Siku si nyingi nitamalizia majimbo ya Urambo na Kaliua kisha Mkoa wa Kigoma. Nimefarijika sana na mwitikio wa wananchi wanaotaka mabadiliko. Wazee kwa Vijana, kina mama kwa kina baba, wanataka mabadiliko.
Nimesononeshwa na kiwango cha umasikini wa wananchi na huduma mbovu za kijamii kama Maji, Elimu na Afya.
Nimeumizwa sana na unyonyaji mkubwa dhidi ya wakulima wa Pamba na Tumbaku.
Nimekasirishwa sana na ufisadi mkubwa wa fedha za umma kupitia mbolea ya ruzuku.
Nina Hofu kubwa ya wanasiasa wengi kutojua changamoto hizi za wananchi lakini wakitaka kupewa dhamana.
Nina Hofu na wanasiasa ‘manipulative’ lakini nina matumaini kuwa viongozi ‘inspirational’ watasimama kidete kushika usukani wa jahazi letu na kulifikisha salama. Tanzania ina kila sababu ya kuendelea, hatuna cha kupoteza isipokuwa minyororo ya umasikini.
Chukua hatua!
VIDEOS Siku ya 8 imetufikisha Jimbo la Nzega-Kamati ya PAC itakagua Mahesabu ya Vyama
Zitto: Kamati yangu PAC itakagua Mahesabu ya Vyama
Zitto: Vijana acheni siasa chafu za kuwachonganisha Viongozi
VIDEOS- Ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi #ChademaTV
Zitto: Mfumo wa Mikopo ya Elimu ya Juu inamnyima haki ya Elimu mtoto wa Mkulima
Zitto: Kwa hali niliyoiona Vijijini inabidi nitafakari upya kustaafu Ubunge
Zitto sijawa Kimya ni Propaganda tu
Siku ya sita ya Ziara ya #CHADEMA imetufikisha Jimbo la Tabora Kaskazini
Siku ya sita ya Ziara ya #CHADEMA imetufikisha Jimbo la Tabora Kaskazini.
Tumefanya mkutano wetu wa mwisho kijijini Mabama. Mkutano mkubwa sana na kuingia wanachama wengi sana. Kilio kikubwa cha wananchi ni Maji na unyonyaji katika zao la Tumbaku. Kuna haja kubwa sana ya kusukuma hifadhi ya jamii kwa wakulima. Tunaweza kukoboa wakulima wengi sana kutoka kwenye unyonyaji.
Ufisadi kwenye ngazi ya kijiji unatisha.
Umewahi kusikia jengo la matofari ya saruji linajengwa kwa tope?
#CHADEMA kanda ya Magharibi leo #Bukene. Kesho 12th Oct #Nzega na keshokutwa 13th #Igunga